Habari za Punde

Serikali Yampongeza Mtawa Kwa Upandaji wa Miti Takriban 160,000

Mtawa wa Mtawa wa Shirika la Yesu Brother Vincent Soleng (wa pili kushoto) akionesha Tuzo ya kutambua mchango wake katika utunzaji mazingira kwa kupanda miti takriban 160,000 aliyopewa na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis ambapo mgeni rasmi wa hafla hiyo alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene. Kulia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Mtakatifu Peter Claver, Padri Karongo Buberwa.
Mtawa wa Mtawa wa Shirika la Yesu Brother Vincent Soleng akitoa neno la shukrani katika hafla ya kumpongeza kwa kupewa Tuzo ya Utunzaji mazingira na Papa Farncis.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akizungumza katika hafla ya kumpongeza Mtawa wa Shirika la Yesu Brother Vincent Soleng mwenye umri wa miaka 83 ambaye amepewa Tuzo na Kiongozi wa Kanisa Katiliki Duniani Papa Francis kutokana na mchango wake katika utunzaji wa mazingira baada ya kupanda miti takriban 160,000 eneo la Ihumwa ilipo Shule ya Sekondari Mtakatifu PeterClaver Jijini Dodoma.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Mtakatifu Peter Claver, Padri Karongo Buberwa akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene kuzungumza.
Sehemu ya wanafunzi wa wa Shule ya Sekondari Mtakatifu Peter Claver wakifuatilia matukio katika halfa ya kumpongeza Brother Vincent Soleng.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mtakatifu Peter Claver wakitoa buridani katika hafla hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akipanda mti ikiwani sehemu ya kumuunga mkono Mtawa Vincent Soleng aliyepanda miti laki sita katika eneo hilo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akiandaa sehemu ya kupanda mti ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Mtawa Vincent Soleng katika juhudi zake za utunzaji mazingira.

Mgeni rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene (mbele katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Dodoma pamoja na wafanyakazi wa Shule ya Sekondari Mtakatifu Peter Claver.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.