Habari za Punde

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Georg Simbachawene.: Mabadiliko ya Tabia Nchi Huathiri Shughuli za Kiuchumi.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Amani Duniani yaliyofanyika Jijini Dodoma.

Na.Mwandishi.OMR.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amesema mabadiliko ya tabianchi nchi huathiri moja kwa moja shughuli za kiuchumi na ustawi wa jamii hivyo huatarisha amani.
Akizungumza kwenye kwenye Maadhimisho ya Siku ya Amani Duniani yaliyofanyika Jijini Dodoma Septemba 21 Mhe. Simbachawene ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kwa kiasi kikubwa mabadiliko ya tabianchi huchangiwa na shughuli za kibinadamu.
Alisema kuwa shughuli hizo husababisha kuongezeka kwa halijoto, kupungua kwa kiwango cha mvua, kukauka kwa vyanzo vya maji na kuongezeka kwa magonjwa ya binadamu, wanyama na mimea.
"Kwa kiasi kiasi kikubwa mabadiliko ya tabianchi huchangiwa na shughuli za kibinadamu zikiwemo uchafuzi wa hali ya hewa, uchomaji misitu, ukataji miti bila kuotesha na shughuli za kilimo na ufugaji zisizozingatia uhifadhi wa mazingira ambazo huchangia kuongezeka kwa hali ya joto," alisema Waziri huyo.
Aliongeza kuwa pamoja na athari za mabadiliko haya kuzikumba nchi zote duniani pia huzikumbwa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania na hi ni kutokana na ukeli kuwa ukuaji wa uchumi wetu hutegemea zaidi shughuli za kiuchumi.
Kutokana na hali hiyo Waziri huyo alibainisha kuwa ili kukabiliana changamoto hizo kama nchi tunahitaji kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ili kuhimili na kujiepusha na majanga yanayosababishwa nayo.
Alitahdharisha kuwa majanga yanayotokana na hali hiyo husababisha hasara za kiuchumi na kijamii zinazochangia kuongezeka kwa umaskini na hata migogoro ya kijamii.
"Chanzo cha kupotea kwa amani kwa baadhi ya maeneo ni chanzo chake ni mabadiliko ya tabianchi na hali ikibadili watu wakakosa mahitaji kama maji hawawezi kukubali kufa lazima watatumia nguvu yoyote kuyapata kwa kugombana.
"Hali ya hewa ikibadilika kusababisha kukosekana kwa maji watu watapambana na kutafuta yake kidogo yaliyopo na katika kuyatafuta lazima watagombana hivyo kusababisha vurugu hivyo amani ina uhusiano mkubwa na mabadiliko ya tabianchi," alisema.
Mhe. Simbachawene alidokeza kuwa Serikali inatambua umuhimu wa mazingira hivyo imeendelea kufanya jitihada kubwa za kutunza na kusimamia mazingira kwa kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa ukuta wa kingo za bahari.
Kwa upande mwingine Waziri Simbachawene alihimiza jumuiya za kimataifa kuweka mkazo katika kukabiliana na janga la mabadiliko ya tabia nchi kwa kuzingatia kuwa uchumi wetu hutegemea shughuli zitokanazo na mazingira.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN)-Tanzania Amon Manyama alipongeza Serikali kwa jiihada zake za kulinda amani hususana katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Alisema kuwa ni jambo jema kuchukua hatua madhubuti za kukabiliana na changamoto hiyo na kuwa amani ni msingi wa kuanzishwa kwa UN hivyo tuhakikishe jitihada hizi zinadumu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.