Habari za Punde

MAKOTI AWATAKA VIJANA KUBUNI MIRADI KATIKA SHEHIA ZAO

Na Khadija  Khamis – Maelezo Zanzibar 22/11/2019
MWENYEKITI wa Baraza la Vijana Taifa  Khamis Haji Kheir ( Makoti) amewataka vijana kubuni miradi mbali mbali ya maendeleo katika Wilaya zao ili kupunguza changamoto za ajira nchini.
Akizungumza katika  mkutano wa utekelezaji wa kazi za Baraza la Vijana  pamoja na kujadili ajenda ya kikao cha baraza la watendaji,kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mkutano wa Baraza la Utamaduni Mwanakwerekwe.
Alisema vijana wachangamkie fursa zilizopo katika Wilaya zao kwani kufanya hivyo kutawasaidia kupata ajira na  kuondokana na utegemezi wa ajira Serikali.
 “Vijana lazima wachangamke kutafuta mbinu za kubuni miradi na wasikate tamaa na hili Serikali ipo tayari kuwaunga mkono katika harakati za kujiinua kiuchumi.” alisema Mwenyekiti .
Hata hivyo alisema Serikali kupitia Baraza la vijana linawasimamia vijana hao zaidi ya 150  kwa  kila wilaya kuwapatia mafunzo  ya ufundi na kuwaongezea ujuzi, uweledi kwalengo la  kupunguza ukali wa maisha.
Aidha alisema Makoti kuna baadhi ya viongozi wa shehia na Wilaya wamechaguliwa kwa kutekeleza majukumu ya kuwasimamia vijana katika kubuni miradi  lakini hutoa visingizio vya kutosaidiwa na baraza na Serikali ,  hivyo hukaa bila ya  kufanya kazi  yeyote jambo ambalo linazorotesha maendeleo.
‘’Kwa mtu ambaye amechanguliwa kuwa kiongozi wa baraza la vijana ambae kazi yake ni kuwasimamia na  kuwasaidia vijana  angalie majukumu yake ya  kazi na kuacha kutoa visingizio visivyokuwa na msingi.”alisema Makoti
Alisema katika kuhakikisha baraza linasonga mbele  limepanga mikakati ya kusimamia vijana kwa kuwaimarisha,katika mafunzo mbali mbali ya ufundi kushirikiana na Serikali ili kufikia malengo ya kuwapatia maendeleo vijana katika nyanja ya kijamii na kiuchumi.
Nae Ofisa Mratibu wa Baraza la Vijana Salum Issa Ameir aliwataka vijana kujitokeza kwa wingi  kujiunga na mabaraza hayo ili kupata fursa mbali mbali zinazojitokeza ikiwemo mafunzo ya ufundi na miradi ya kimaendeleo.
Kikao hicho kilihusisha vipengele tofauti vya utekelezaji wa baraza hilo ikiwemo  ushauri, mipango  ya  ajira kwa vijana,pamoja na kuyaimarisha mabaraza ya vijana Wilaya Shehia na hadi Taifa  A

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.