Habari za Punde

Mmiliki wa Nyumba ya Kulala Wageni Pemba Ametoa Wiki Moja kwa ZFF Kulipwa Fedha Zake.


Na. Abdi Suleiman - Pemba.
MENEJA wa Pataya Guest house ya Machomanne Chake Chake Pemba, Said Seif Said amesema kuwa anatowa wiki moja kwa shirikisho la Mpira Zanzibar (ZFF), kumlipa fedha zake za waamuzi waliokuwa wakilala katika hoteli hiyo, vyenginevyo anakwenda kwenye vyombo vya sheria kudai haki yake.

Said alisema kuwa wiki hiyo ni kuanzia Disemba 29 mwaka 2019, ikipita atakipeleka chama hicho katika vyombo vya dola kwa kudai malipo ya waamuzi hao, kwani ni miezi mingi imepita bila ya kupata haki yake licha ya kuwasiliana na viongozi wakuu wa chama hicho.

Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari za michezo, katika ofisi za gesti hiyo iliyopo mtaa wa machomanne Chake Chake Pemba.

Aidha meneja huyo aliwataja waamuzi hao, ambao wamelala na kutokulipwa fedha zake kiasi cha shilingi laki 315000 kwa siku tisa ambacho chumba kwa siku ni shilingi 35000, kuwa ni Mfaume Ali, Mohd Mwalim, Mbaraka Haule na Issa Haji.

Alisema dhamana ya malipo ya waamuzi alikubaliana na Mwenyekiti wa kamati ya waamuzi Kibabu Haji, juu ya malipo na mwanzo walipokuwa wakilala walikwenda vizuri, baadae ndio maharibiko yalipoanza pale walipokuwa wakilala siku tano wanalipwa tatu na mwisho hajalipwa kabisa.

"Ndugu waandishi kama hawajinipa pesa zangu na hali ikaendelea kuwa hivi, mimi nitaenda kwenye vyombo vya sheria kudai haki yangu, nimeshadai sana na hakuna linaloendelea mpaka sasa" alisema.

“Mwanzo walikaa siku Tanoa wakalipa siku tatu, halafu wakaa siku mbili, hawakuliza zikawa siku nne, halafu wakaja tena wakakaa siku tano, zitakuwa siku Tisa na wanakuja waamuzi wawili wawili, zote hizo mimi sijalipwa mpaka sasa’alisema.

Aidha alisema tayari jutihada mbali mbali alishazifanya, ikiwemo kuwasiliana na wahusika juu ya kupata haki yake, lakini mpaka sasa hakuna jibu sahihi juu madai yake kupatiwa.

Said alifahamisha jitihada nyengine alizichukuwa kwa kuwasiliana na rais wa chama hicho, kwa njia ya ujumbe mfupi wa sms baada ya kuona simu haipokeliwi, jambo ambalo limemrudisha nyuma kimaendeleo ikizingatiwa mwanzo walikubalia vizuri juu ya malipo.

Hata hivyo alisema kibaya zaidi fedha hizo ni fedha za taasisi ambayo inalipa Kodi, zinatumika kwa ajili ya kuendeshea shuhuli na sio kuishia mikononi mwa mtu au taasisi.

Katibu wa shirikisho la soka Zanzibar (ZFF) Mohamed Ali Hilali (Tedy), alikiri kulifahamu deni hilo huku akiahidi kuwa uongozi utahakikisha unalilipa haraka iwezekanavyo.

Mwenyekiti wa kamati ya waamuzi Zanzibar, ambaye pia ndie aliekuwa akichukuwa dhamana ya malipo ya waamuzi hao, Kibabu Haji akiri kulifahamu deni hilo na kudai kuwa tayari alishaliwasilisha katika chama husika kwa ajili ya utekelezaji.

Alisema yeye jambo hilo sio la kwake bali ni la taasisi husika, hivyo majukumu yake ya kiutendaji baada ya kumaliza aliliwasilisha kwa uongozi, kwani hata wakati akipatiwa malipo yake huko mwanzo taarifa zilifika kwa wahusika.

“Baada ya kupatiwa malipo yake huko mwanzoni pia stakabadhi za malipo aliweza kutoa, hicho ambacho hakikupatikana nilitoa muongozo wote ili kupatiwa haki zake”alisema kibabu.

Hata hivyo alimtaka Mmiliki huyo kuendelea kuwasilina na viongozi wajuu wa soka ili kuona haki zake anapatiwa kwa njia gani, kuliko kukimbilia kwenye vyombo vya sheria.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.