Habari za Punde

ZSSF KUTOA MABATI 50 KATIKA SKULI YA MSINGI MWEMBESHAUR

Na. Kijakazi Abdalla. 
Mfuko wa Hifadhi Zanzibar (ZSSF) umekabidhi msaada wa mabati 50 kwa Skuli ya  na Maandalizi Mwembeshauri kwa ajili ya kuezekea banda la skuli hiyo.
Akikabidhi msaada huo Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya  (ZSSF) Ali Suleiman Ahmada amesema kuwa msaada huo  ni kwa ajili ya ujenzi wa darasa la Skuli ambalo  linavuja.
Amesema kuwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) umekabidhi msaada huo  baada ya kupata  maombi kutoka kwa Muakilishi wa Jimbo hilo Nassor Salum Jazeera wa kutaka  kusaidia mabati .
Aidha amesema kuwa lengo la mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) ni kurejesha huduma kwa jamii ili kuona mfuko huo unawanufaisha  wananchi wake katika Nyanja za elimu pamoja na afya.
Hata hivyo ameitaka jamii kuzidisha nguvu zaidi katika kuchangia katika mfuko huo ili kuwekeza kwani kuekeza ni moja ya kujiekea nguvu hapo baadae
Nae Mwalimu  Msaidizi wa Skuli ya Mwembeshauri Mgeni Rajabu Khamis ameushukuru Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) kwa msaada walioutoa  kwani umekuja kipindi muafaka.
Aidha amesema kuwa msaada huo utazidisha nguvu kwa walimu ya kujenga  ari ya ufundishaji kwa kuwapatia wanafunzi elimu bora ambayo inahitajika katika skuli hiyo.
“Msaada umekuja kipindi muafaka utatuzidishia nguvu zaidi ya kufundisha na wanafunzi watasoma katika mazingira yaliyo bora”alisema  Mwalimu Mgeni.
Nae Muakishi wa Jimbo la Kikwajuni Nassor (Jazeera) ameitaka jamii kuzidisha nguvu za kuchangia mfuko huo ili kupata manufaa hapo baadae
Aidha amezitaka taasisi nyengine wajitokeze  kuiga mfano kama huo  wa kusaidia jamii  hasa katika Nyanja ya elimu  kwani kuekeza katika njia moja ya kujiengezea uwezo.  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.