Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein Atumaa Salamu za Rambirambi Kwa Sultani wa Oman .Sultan Haitham Bin Tariq Al Said Kufuatli Kifo cha Kiongozi wa Oman.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, amemtumia salamu za rambirambi Sultan wa Oman,Sultan Haitham Bin Tariq Al Said kufuatia kifo cha kiongozi wa nchi hiyo Sultah Qaboos bin Said Al Said.

Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Shein alieleza kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Sultan Qaboos bin Said Al Said aliyefariki Januri 10, 2020 akwia na umri wa miaka 79.

Salamu hizo ziliendelea kuweleza kuwa kwa niaba ya wananchi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na yeye mwenyewe binafsi, Rais Dk. Shein anatuma salamu za rambi rambi kwa serikali, familia pamoja na ndugu jamaa pamoja na wananchi wote wa Oman kufuatia kifo cha kiongozi wao huyo.

Aidha, salamu hizo ziliongeza kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana na ndugu zao wa Oman katika msiba huo mzito wa kiongozi huyo na kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Sultan Qaboos mahala pema peponi,Amin.

Sambamba na hayo, salamu hizo zilieleza kuwa kumbukumbu ya mafanikio na mchango mkubwa alioutoa Sultan Qaboos katika maendeleo ya Oman na duniani kwa jumla yataendelea kukumbukwa daima kwa Oman pamoja na wapenda amani wote duniani.

“Namuomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira ndugu, jamaa, wanafamilia na wananchi wote wa Oman katika kipindi hichi kigumu cha msiba”, ilieleza sehemu ya taarifa hiyo ya rambirambi aliyoituma Rais Dk. Shein.

Sultan Haitham Bin Tariq Al Said ambaye alikuwa Waziri wa Utamaduni na thurathi za kitaifa ameapishwa siku ya Jumaamosi baada ya mkutano wa Baraza la Familia ya Kifalme kuwa mrithi wa Sultan Qaboos.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.