Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na mgeni wake Katibu Mtendaji wa SADC Dkt.Stergomena Lawrence, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza mgeni wake Katibu Mtendaji wa SADC Dkt.Stergomena Lawrence, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na mgeni wake Katibu Mtendaji wa SADC Dkt. Stergomena Lawrence Tax, alipofika Ikulu kwa mazungumzo yaliofanyika leo 21-2-2020 , katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Dk. Shein amesema
hayo Ikulu Jijini Zanzibar, alipokutana na Katibu Mtendaji wa SADC Dkt.
Stergomena Lawrence Tax aliefika kwa ajili ya kusalimiana nae.
Alisema nchi wanachama
wa SADC zinakabiliwa na changamoto mbali mbali zinazofanana, zikiwemo za
majanga pamoja na za kiuchumi, hivyo ni vyema zikashirikiana katika kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo.
Akigusia suala la
suala la majanga, Dk. Shein alisema ni changamoto inayoikabili dunia nzima, ambapo
hutofautiana kulingana na mazingira ya kimaeneo.
Alisema kufanyika
kwa mkutano wa kwanza wa Kamati ya Mawaziri wenye dhamana ya Menejment ya Maafa
kwa nchi wanachama wa SADC ni mwanzo
mzuri katika muelekeo wa kuzipatia ufumbuzi baadhi ya changamoto hizo.
Alisema Zanzibar
kwa upande wake imeanza kulitafutia ufumbuzi tatizo la kutuwama kwa maji ambalo
husababisha majanga, (hususan katika maeneo ya ng’ambo) kwa kujenga mitaro
mikubwa inayopeleka maji moja kwa moja baharini.
Aidha, Rais Dk.
Shein alisema kuna haja kwa nchi wanachama wa SADC kutafakari namna gani zitakavyoshirikiana
na kusaidiana katika dhana ya kuimarisha uchumi wa nchi zao, kwa kubadilishana
uzoefu pamoja na uapatikanaji wa mafunzo.
Alisema kuna
umuhimu wa nchi hizo kubadilishana bidhaa hususan zitokanazo na kilimo kwa njia
ya kuuziana, ikiwa ni hatua itakayopunguza gharama.
Akigusia matumizi
ya lugha ya Kiswahili kwa nchi wanachama, Dk. Shein alisistiza umuhimu wa nchi
za SADC kuwa na utaratibu na mikakati ya kuanza matumizi ya lugha hiyo, na
kuipongeza Burundi kwa mafanikio iliyofikia katika matumizi ya kiswahili.
“Ni vyema kila
nchi ikajitayarisha kutumia Kiswahili, lazima ianze kwa maeneo”, alisema.
Aidha, Dk. Shein
alibainisha dhamira ya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano na ile ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika kusimamia Demokrasia nchini kwa kuzingatia sheria na Katiba za
nchi.
Mapema, Katibu
Mtendaji wa SADC Dkt. Stergomena
Lawrence Tax, aliishukuru Serikali kwa kukubabali kuaanda mkutano huo muhimu,
hatua aliyosema inatokana na kutambua mchango mkubwa wa Tanzania katika
maendeleo na mustakbali wa Jumuiya hiyo.
Alisema hali ya
ulinzi na usalama kwa nchi wanachama wa SADC ni nzuri mbali na kuwepo kwa
matukio mbali mbali yanayojiri kabla na baada ya chaguzi.
Alishauri
kutiliwa mkazo suala la upatikana wa ajira kwa vijana katika nchi wanachama ili
kuondokana na kadhia mbali mbali zinazojitokeza.
Aidha, Dkt
Lawrence aliipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, chini ya Uongozi wa Dkt
Shein kwa maendeleo makubwa ya kiuchumi na kijamii iliyofikia, hivyo akabainisha
azma ya SADC ya kuunga mkono juhudi hizo.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment