Habari za Punde

Ukaguzi wa Abiria Wanaowasili Uwanja wa Ndege wa JNIA Kudhibiti Virusi Vya Corona

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalim (aliyenyoosha mkono) akimwelekeza eneo la ukaguzi wa afya Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Florens Turuka alipowasili leo nchini katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Florens Turuka akinawa mikono kwa dawa maalum eneo la ukaguzi wa afya alipowasili nchini leo katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). Hiyo ni moja ya kujikinga na virusi vya homa ya mapafu ya Corona iliyotokea nchini China.
Afisa Afya Mkuu Mazingira, Onesmo Kitange (wsa pili kushoto) leo akizungumza na Mhe Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee  na Watoto wakati alipotembelea Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), kujionea udhibiti wa homa ya mafua inayosababishwa na virusi vya Corona.
Eneo maalum la kusimama abiria wanaowasili nchini wakitokea nchi mbalimbali kwa ajili ya ukaguzi wa afya, endapo watagundulika na homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona, iliyoanzia nchini China.

Mtawa Michaela Chaudrasekar kutoka nchini India, akipimwa joto la mwili kwa kutumia kifaa maalum cha mkono na Afisa Afya Mkuu Mazingira, Onesmo Kitange alipowasili nchini leo kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA, ili kutambua endapo ameambukizwa virusi vya homa ya mapafu aina ya Corona vilivyoanzia nchini China.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.