Habari za Punde

KATIBU MKUU KADIO AWAONGOZA WATENDAJI WAKUU MAGEREZA KIKAO CHA KAMATI YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA, WAJUMBE WAKAGUA UJENZI KIWANDA CHA USEREMALA, MSALATO DODOMA

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio, akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kabla ya Kamati hiyo kupokea taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Useremala cha Magereza, Msalato Mkoani Dodoma, leo. Wajumbe hayo walitoa ushauri wa kuboresha ujenzi wa Kiwanda hicho ambao tayari umenza. 
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Salim Mwinyi Rehani, akizungumza katika kikao cha Kamati hiyo kilichojadili Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Useremala cha Magereza, Msalato Mkoani Dodoma, leo. Wapili kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio. Kushoto ni Katibu wa Kamati hiyo, Ramadhani Abdalla, na kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Suleiman Mzee. 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio (kulia), akisalimana na Katibu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Ramadhani Abdalla, wakati alipokuwa anawasili na Wajumbe wa Kamati hiyo kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Useremala cha Magereza, Msalato Mkoani Dodoma, leo
Mhandisi wa Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Useremala cha Magereza, Bonaza Malata (kulia), akiwaonyesha Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Ujenzi wa Kiwanda hicho kilichopo Msalato Mkoani Dodoma, leo. Kamati hiyo ilipokea taarifa ya Mradi huo ambao tayari umeanza na kutoa ushauri wa kitaalamu wa ujenzi wa Kiwanda hicho. Wapili kulia ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Salum Mwinyi Rehani, na watatu kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio. 

Mhandisi wa Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Useremala cha Magereza, Bonaza Malata (kulia), akiwafafanulia jambo Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kuhusu Ujenzi wa Kiwanda hicho kilichopo Msalato Mkoani Dodoma. Kamati hiyo ilipokea taarifa ya Mradi huo ambao tayari umeanza na pia kutoa ushauri wa kitaalamu wa ujenzi wa Kiwanda hicho. Watatu kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Salim Mwinyi Rehani, na kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.