Naibu Waziri Wizara
ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo mheshimiwa Juliana Shonza akimsisitiza
msanii wa bongofleva Rashid Abdallah maarufu kama Chid benz kufanya kazi kwa
bidii na kuwa mbunifu huku akimhakikishia kuwa serikali ipo tayari kumpa
ushirikiano alipokuwa akifanya kikao nae leo jijini Dodoma.
Msanii wa bongofleva
nchini Rashid Abdallah maarufu kama Chid benz akimweleza Naibu Waziri Wizara ya
Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo mheshimiwa Juliana Shonza (kulia) kuwa
mapema wiki ijayo anatarajia kutoa video ya wimbo wake wa Beautiful na pia
atatunga wimbo wa kuhusu Corona katika kikao kilichofanyika leo jijini Dodoma.
Naibu Waziri Wizara
ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo mheshimiwa Juliana Shonza akiwa
akimsisitiza msanii wa bongofleva Rashid Abdallah maarufu kama Chid benz kuwa
wizara ipo tayari kumpa ushirikiano wakati wowote na kikubwa ni msanii huyo
kujituma na kuonyesha umma kweli ameachana na matumizi ya madawa ya kulevya
mara baada ya kikao leo jijini Dodoma.
Na Anitha Jonas –
WHUSM Dodoma.
Naibu Waziri Wizara
ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza amwaahidi ushirikiano
msanii wa bongofleva nchini Rashid Abdallah maarufu Chidbenz.
Mheshimiwa Shonza
ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma alipofanya kikao na msanii huyo ambapo Chid
benz alimuhakikishia kuwa kwa sasa
amebadilika na anataka kuwaonyesha watanzania amefanikiwa kujikwamua
katika matumizi ya madawa ya kulevya na hataki tena kurudi huko kwani anazaidi
ya miezi mitatu sasa hajatumia madawa hayo kabisa.
“Kati ya wasanii
wenye kukubalika na mashabiki zao wewe
Chid benz ni mmoja wao na mashabiki zako
ni wengi hivyo ningependa kukuona kwanzia sasa unalijenga zaidi jina lako kwa kuonyesha kuwa
umebadilika,katika kipindi hichi nitafurahi zaidi kukuona unasonga mbele na
hurudi tena katika matumizi ya madawa ya kulevya wizara ipo pamoja na wewe kukusaidia wakati wowote ,”alisema
Mhe.Shonza.
Akiendelea kuzungumza
katika kikao hicho mheshimiwa Shonza
alimsisitiza msanii huyo kuwaonyesha watanzania kuwa anaweza na hata akipewa nafasi
anaweza kujitumia vyema na kuonyesha
juhudi yake katika kufanya kazi na kuwa mbunifu katika kufanya kazi zake za
usanii.
Naye Msanii huyo wa
Bongofleva Chid benz alieleza kuwa kwa sasa hautarudi nyuma tena sababu tayari
amekwisha acha kutumia matumizi ya
madawa hayo na ninaelewa bahati haiji mara mbili lakini kwangu naiona imekuja
zaidi ya mara moja kwa maana ya kuwa nimekuwa nimekuwa na anguka nainuka narudi
kwa mashabiki wananipokea nakuendelea kukubali muziki wangu hakika najiona
niwakati wa kuwafurahisha zaidi mashabiki na sitawaangusha.
“Ombi langu kwa
serikali ni kupata ushirikiano na mapema wiki ijayo ninatarajia kutoa wimbo
wangu mmoja uitwao Beautiful ambao nimeuiamba nikisifu uzuri wa mwanamke na
kufuatia janga la Corona ninamwahidi mheshimiwa Naibu Waziri kuwa nitatunga
wimbo kwa ajili ya Corona ,”Chid benz.
Pamoja na hayo nae
Chid benz alitoa wito kwa watanzania kuacha kufanya mzaha katika mitandao ya
jamii kuhusu suala la ugongwa Corona sababu hili ni tatizo ni janga
linalosumbua dunia kwa sasa hivyo jambo la msingi ni kuzingatia maelekezo
yaliyotolewa na serikali kutoka kwa wataalamu wa afya.
No comments:
Post a Comment