Washiriki wa mkutano wa siku moja (1) ulioandaliwa na MISA-Tan uliojadili, pamoja na mambo mengine ,umuhimu na changamoto za uhuru wa kujieleza na kupata taarifa nchini Tanzania.
Mshiriki Bw. Joseph Kavishe kutoka mamlaka ya mawasiliano Tanzania(TCRA) akichangia mjadala kuhusu makosa ya mtandao na sheria zake wakati wa kikao cha majadiliano kilicho andaliwa na MISA-Tan.
Haji Mtumwa, Zanzibar
Mshiriki Bw. Joseph Kavishe kutoka mamlaka ya mawasiliano Tanzania(TCRA) akichangia mjadala kuhusu makosa ya mtandao na sheria zake wakati wa kikao cha majadiliano kilicho andaliwa na MISA-Tan.
Haji Mtumwa, Zanzibar
Imeelezwa kuwa tokea kuanzishwa kwake Taasisi ya vyombo vya
habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania (MISA-Tan) imekua ikipigania uhuru wa
kutoa maoni na uhuru wa vyombo vya Habari.
Hayo yamebainika katika mkutano wa siku moja ulioandaliwa
na MISA-Tan uliojadili umuhimu na
changamoto za uhuru wa kujieleza na
kupata taarifa nchini Tanzania, mkutano ambao umeongozwa na Mjumbe wa Bodi ya
MISA-Tan, Michael Gwimile.
Moja wapo ya changamoto ilielezwa katika mkutano huo ni uhuru wa kutoa maoni na kupata taarifa ni
uwepo wa sheria mbalimbali, sheria hizo ni pamoja na sheria ya huduma za vyombo
vya Habari, sheria ya makosa ya mtandao na sheria ya takwimu.
Kwa bahati mbaya waandishi wa Habari na wananchi kwa ujumla
wana uelewa mdogo juu ya sheria hizi, mfano mzuri kumekuwa na ongezeko la
makosa yatokanayo na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na hivyo kupelekea
kuvunja sheria ya makosa ya mtandao.
Baadhi ya wahanga ni mwandishi wa Habari wa gazeti la
Tanzania Daima tokea Zanzibar Bw. Talib ussi Hamad, aliesimamishwa kufanya
shughuli za uandishi wa Habari kwa muda wa miezi sita baada ya kutoa taarifa
kwenye ukurasa wake wa facebook akimtangaza mwandishi mwenzake kuwa ana corona.
Changamoto za uhuru wa kujieleza na kupata taarifa
zimepelekea MISA-Tan kuandaa mkutano wa wadau mbalimbali wa vyombo vya Habari
ili kujadili namna bora ya kuongeza uelewa juu ya namna sahihi ya kutumia
mitandao ya kijamii.
Katika mkutano huo maswala kadhaa yalijadiliwa ikiwemo
kutumia vyanzo sahihi vya taarifa na waandishi
na wananchi kujiridhisha na usahihi wa taarifa wanazopokea kabla ya
kuzisambaza.
No comments:
Post a Comment