Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi akizungumza wakati wa hafla ya Kongamano la UWT 2Umoja Wetu Wanawake Ndio Nguvu Yate" lililofanyika katika ukumbi wa Afisi ya CCM Mkoa wa Mjini Kichama Amaniu Jijini Zanzibar.
MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi ameahidi kuwa nafasi nyingi za
uteuzi katika Serikali atakayoiunda ya Mapinduzi ya Zanzibar wanawake watapewa
kipaumbele kwani ndio nguzo ya chama hicho.
Dk. Hussein aliyasema hayo leo wakati akitoa salamu
katika Kongamano maalum la Wanawake lililofanyika katika ukumbi wa Amani CCM Mkoa,
ambapo Mgeni Maalum katika Kongamano hilo alikuwa Mke wa Rais wa Zanzibar Mama
Mwanamwema Shein na Mgeni Rasmi alikuwa Mwenyekiti wa (UWT) Gaudentia Mugosi
Kabaka.
Katika salamu zake hizo, Dk. Hussein Mwinyi
alisema kuwa anauhakika mkubwa kwamba CCM itashinda kutokana na wagombea wake wa
uongozi kuungwa mkono na makundi yote ndani ya chama hicho wakiwemo wanawake
ambao ndio jeshi kubwa la CCM.
Alisema kuwa wanawake wamekuwa wakifanya vizuri
pale wanapopewa nafasi ya uongozi kwani wamekuwa wakionesha uadilifu wao
mkubwa.
Dk. Hussein alieleza kuwa katika kampeni zote za
CCM wahamasishaji wakubwa ni wanawake ambao mara zote wamekuwa kitu kimoja
katika kukiunga mkono na kukitetea chama chao cha CCM.
Aliongeza kuwa umefika wakati wagombea wote
wanawake wa CCM waliogombea nafasi mbali
mbali zikiwemo za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani kuwa kitu kimoja ili
kuhakikisha chama chao kinaendelea kuongoza dola na kupata ushindi wa kishindo.
Katika salamu zake hizo Dk. Hussein Mwinyi alitoa
wito kwa wanawake kuendelea kukitetea chama hicho na kuhakikisha kinapata
ushindi na kuweza kuongoza Serikali.
Aidha, Dk. Hussein alieleza kuwa kampeni kubwa za
chama hicho zitafanywa majukwani lakini zaidi zitafanywa katika mikutano ya
ndani.
Sambamba na hayo, Dk. Hussein Mwinyi alisisitiza
haja ya kuendelea kuitunza amani kwani bila ya amani hakuna maendeleo.
No comments:
Post a Comment