Habari za Punde

Inna Lillah wa Inna Ilayhi Rajiuun Mgombea Ubunge Jimbo la Mpendae Kupitia CCM Mhe. Salim Hassan Abdullah Turky ( Mr. White)

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mpendae  na Mgombea Ubunge Jimbo la Mpendae Zanzibar Mhe. Salim Turky, akitambulishwa wakati wa uhai wake katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CCM  zilizofanyika katika Uwanja wa Demokrasia Kibanda Maiti  jumamosi 12/9/2020  wiki iliopita.

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mpendae na Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo Mhe. Salim Hassan Abdallah Turky (Mr. White) amefariki dunia jana usiki katika Hospitali ya Global Jijini Zanzibar 

Kwa mujibu wa wawakilishi wa familia maziko yatafanyika leo 15/9/2020  nyumbani kwake Mpendae Jijini Zanzibar  saa kumi baada ya sala ya Alasri  na kusaliwa katika Masjid Noor Muhammad Kwa Mchina na anatarajiwa kuzikwa katika makaburi ya Fuoni Kijitoupele.

Inshaalah Mwenyenzi Mungu ampe kauli thabi  na kumsamehe madhambi yake 
Ameen.

Inna  Lillah wa Inna  IIayhi Rajiuun 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.