Habari za Punde

Wajumbe wa Baraza Wawakilishi waendelea na semina elekezi

Balozi Mstaafu Dkt Mahadhi Juma Maalim akiwasilisha mada inayohusu mgawanyo wa madaraka na kazi za baraza la wawakilishi katika semina elekezi kwa wajumbe wa baraza la 10 la wawakilishi

Jaji Mkuu Wa Zanzibar, Omar Othman Makungu akiwasilisha mada inayohusu uhusiano wa Baraza la Wawakilishi  na mihimili mengine katika mafunzo elekezi kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi yanayofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani

Jaji Mkuu Wa Zanzibar, Omar Othman Makungu akiwasilisha mada inayohusu uhusiano wa Baraza la Wawakilishi  na mihimili mengine katika mafunzo elekezi kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi yanayofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani

Jaji mkuu wa Zanzibar Mhe, Omar Othman Makungu amesema kuna umuhimu mkubwa wa mihimili mitatu ya dola kushirikiana  katika utendaji wa kazi zao ili kuweza kuwahudumia vizuri wananchi katika kuwaletea maendeleo.

Jaji Othman makungu ameyasema hayo wakati akiwasilisha mada ya “uhusiano wa Baraza La Wawakilishi na mihimili mengine” katika mafunzo elekezi kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi yanayoendelea katika ukumbi wa Baraza hilo Chukwani.

Amesema lengo kubwa la vyombo hivyo ni kugawana madaraka katika kutoa huduma bora kwa wananchi katika misingi ya demokrasia ambapo malengo hayo hayatofikiwa ikiwa  vyombo hivyo vitakua na migogoro ndani yake.

Amefahamisha kuwa kwa upande wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla vyombo hivyo vitatu vinafanya kazi kwa mashirikiano makubwa ambayo yameipelekea serikali kuleta maendeleo makubwa kwa wananchi wake.

Wakati huo huo balozi  mstaafu  Dkt Mahadhi Juma Maalim akiwasilisha mada inayhusu “mgawanyo wa madaraka na kazi za Baraza la wawakilishi” amewasisitiza wajumbe wa baraza hilo kujifunza  kwa umakini sheria na kanuni zinazoongoza utendaji wa kazi wa baraza pamoja na kuwatumia wataalamu wa baraza hilo kuweza kutekeleza majukumu yao kwa uweledi mkubwa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.