Habari za Punde

ZEC Yawatangaza Wajumbe wa Viti Maalum Vya Wanawake.

Na JaalaMakame Haji - ZEC

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC imewatangaza wajumbe kumi na nane 18 kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa nafasi za Viti Maalum vya Wanawake vya Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar. 

Tume imetangaza majina ya Wajumbe hao katika Mkutano wake uliofanyika leo 07/11/2020 katika ukumbi wa mikutano wa Tume hiyo Maisara Jijini Zanzibar.

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imewatangaza wajumbe 18 kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa mujibu wa masharti na maelekezo ya Ibara ya 67 ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984.

Aidha Tume imewatangaza wajumbe hao baada ya kuridhika kuwa wote wana sifa ya kuwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kama zilivyoainisha katika Katiba ya Zanzibar Ibara ya 68.

Waliotangazwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ni

1.Bi.Panya Ali Abdallah.

2 Bi. Bihindi Hamad Hassan.

3.Bi.Salma Mussa Bilal.,

4.Bi.Shadya Mohammed Suleiman. 

5, Bi.Fatma Ramadhan Mohamed (Mandoba).

6. Bi.Saada Ramadhan Mwenda.

7. Bi.Mwantatu Mbaraka Khamis.

8.Bi.Zainab Abdalla Salum.

9. Bi.Riziki Pemba Juma.

10. Bi.Leila Mohamed Mussa.

11. Bi.Salha Mwinyi Juma.

12. Bi.Hudhaima Mbarak Tahir.

13. Bi.Sabiha Fil fil Thani.

14. Bi.Aza Januar Joseph.

15. Bi.Mwanaid Kassim Mussa.

16. Bi.Mgeni Hassan Juma.

17. Bi.Mwanajuma Kassim Makame.

18. Bi.Rahma Kassim Ali.

Tume tayari imeshawasilisha Majina ya Wajumbe hao kwa Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kwa ajili ya Hatua nyengine za Kisheria.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.