STATE HOUSE
ZANZIBAR
OFFICE OF THE
PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
11.01.2021
RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa msamaha kwa wanafunzi (wafungwa) Arobaini na Tisa (49) waliokuwa
wakitumikia Vyuo vya Mafunzo vya Unguja na Pemba ikiwa ni miongoni mwa shamra
shamra za Sherehe za miaka 57 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Dk. Mwinyi ametoa msamaha huo kwa mujibu wa
kifungu cha 59 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kinachompa mamlaka ya
kutoa msamaha kwa wafungwa waliofungwa gerezani.
Kutokana na msamaha huo, Dk. Mwinyi ameamuru
kuwa kifungo kilichobaki cha wanafunzi (wafungwa) hao walionufaika na msamaha
katika vyuo vya Mafunzo vya Unguja na Pemba kuwa kipindi hicho chote kinafutwa
na waachiwe huru kuanzia Januari 11.2021.
Kwa vile, Zanzibar itakuwa inasherehekea miaka 57 ya
Mapinduzi Matukufu ya Januari 12, 1964 Dk. Mwinyi ameona kuwa kuna sababu za
kutosha za kutoa msamaha kwa walengwa walionufaika na msamaha huo kwa Unguja ambao ni 46 na Pemba 3.
Msamaha huo hutolewa kila mwaka katika
kipindi cha sherehe za Mapinduzi matukufu, huwahusisha wanafunzi ambao ni wazee
sana, wenye maradhi sugu au wenye makosa madogo ambao wamebakisha muda mfupi wa
kutumikia chuoni, wanaoonesha nidhamu nzuri chuoni na kujutia makosa yao.
Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo, wenye makosa
kama vile kuua kwa makusudi, wizi wa kutumia nguvu, wizi wa mali ya Umma,
makosa ya kudhalilisha wanawake na watoto, makosa ya dawa za kulevya na wenye
makosa mengi ya zamani kwa kawaida huwa hawapewi msamaha.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
No comments:
Post a Comment