Habari za Punde

TAMWA, ZNZ, yampongeza Mkurugenzi wake Dr. Mzuri Issa


Chama Cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, Zanzibar, (TAMWA ZNZ) tunapenda  kumpongeza Mkurugenzi wetu  Dr. Mzuri Issa kwa kupata tunzo  ya kutoa mchango mkubwa katika jamii kwenye maisha yake. Tunzo hizo zimeolewa na waandaaji wa Tunzo za Vijana Zanzibar (ZYA) hii ikiwa ni mara ya pili mfululizo.

Mkuu wa jopo la majaji Bw Rashid Mohammed Rashid, alisema mara hii pamoja na kuitoa zawadi kwa vijana wameona pia watowe tunzo kwa watu waliosaidia sana maendeleo ya vijana nchini.

Wengine wanne walipewa tunzo hizo ni Daudi Kombo Maalim, Shaib Ibrahim Mohamed, Raza Lee na DJ Saleh katika ghafla iliyohudhuriwa na Waziri wa Habari, Vijana Mh Tabia Mwita huko Michenzani Mall jana usiku.

 Dr. Mzuri amepata tunzo hiyo kutokana na kuwawezesha vijana wanawake katika nyanja mbali mbali za kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.