Habari za Punde

Ufungaji wa Kongamano la pili la Amani Zanzibar Beach Resort Mazizini Zanzibar

 Mufti Mkuu wa Rwanda Shekh Saleh Habimana  akitoa mada kwa washiriki wa Kongamano la Amani akitoa muongozo kuilinda amani ya Zanzibar kupitia mafundisho yaliomo ndani ya Quran na historia ya maisha ya Mtume Muhammad (s.a.w) huko  Mazizini nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Washiriki wa Kongamano la Amani wakisikiliza kwa makini mada mbambali zilizowasilishwa katika kongamano ambapo washiriki kutoka Afrika Mashariki na nje ya Afrika walishiriki Kongamano lililofanyika Zanzibar Beach Resort Mazizini Zanzibar.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria na Utawala bora Haruna Ali Suleiman akifunga Kongamano la Amani la siku mbili  lililofanyika katika ukumbi  wa Hoteli ya  Zanzibar Beach Resort Mazizini Zanzibar. 


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria na Utawala Bora Haruna Ali Suleiman akiwa katika picha ya pamoja na Marafiki wa Amani wa Zanzibar wanaotoka nje ya Zanzibar katika Kongamano la Amani  lililofanyika katika ukumbi  wa Hoteli ya  Zanzibar Beach Resort Mazizini Zanzibar. 


Picha na  Bahati Habibu Maelezo Zanzibar

Na Miza Kona   Maelezo/ Zanzibar    18/01/2021

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora Mhe. Haroun Ali Suleiman amesema Zanzibar ni nchi yenye historia ya amani hivyo ni vyema jamii ikaendelea kujenga amani na kudumisha mashirikiano yaliyopo nchini.

Waziri Haroun ameyasema hayo huko Zanzibar Beach Resort wakati wa ufungaji wa Kongamano la Pili la Kitamatafa la Amani, amesema kudumisha amani ni jambo la msingi katika kutekeleza majukumu na kuleta maendeleo.

Ameeleza kuwa maridhianio yaliopo yameleta mafanikio makubwa nchini kwani yameweza kuleta umoja, mshikamano na kuunganisha udugu wa kihistoria katika jamii ya wazanzibari ambayo duniani kote imelifurahia jambo hilo.

Waziri Haroun amesisistiza kuidumisha amani ndani na nje ya nchi ili Zanzibar ibaki kuwa na historia yenye amani na utulivu na kigezo kwa wengine.

Pia Waziri Haroun amewashukuru marafiki wa Zanzibar kuweza kuilinda na kuidumisha amani nchini na kuwataka kuendelea kuiunga mkono katika kuleta maendeleo.

Mapema akiwasilisha Mada ya Vijana baada ya Uchaguzi Mwezeshaji Sheikh Ibrahim Lethome Wakili kutoka Mahkama Kuu ya Kenya amesema vijana ni lazima walelewe katika maadili mazuri ya dini na kupewa fursa ili kuepukana na ushawishi wa kiasiasa na kuwa mabalozi wazuri wa kudumisha amani.

“Utaratibu wa kuwalea vijana lazima vijana walelewe katika misngi ya dini, wawe na huruma, jasiri na kuutumia vizuri ujana wao wawe na subira, vijana pia wapewe fursa za kujiendeleza kimaisha” alifahamisha Mwezeshaji huyo.

Nae Mwezeshaji Ramadhan Haula akitoa mada ya Mchango wa Vyombo vya Habari katika kulinda amani na utulivu amesema vyombo vya habari vina uwezo mkubwa wa kudumisha amani kwani ni kifaa kinachofikisha ujumbe kwa jamii na kutoa matukio mbalimbali yanayotokea duniani.

Amefahamisha kuwa chombo cha habari ni chombo chenye kutoa mawasiliano na jamii hivyo kinaushawishi mkubwa wa kudumisha ama kuvuga amani ni lazima vitumike vizuri katika kudumisha amani na utulivu nchini.

Kongamano hilo la Kimataifa la siku mbili ambalo limeshirikisha nchi marafiki wa Zanzibar ikiwemo Mozambique, Malawi, DR Congo, Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya Tanzania Bara, Norway, Switzierland na Germany     

   

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.