Habari za Punde

Maofisa Mawasiliano Watakiwa Kuelimisha Jamii Kuhusu Huduma Zinazotolewa na ZURA.

Na Miza Kona Maelezo Zanzibar. 20/05/2020

Maafisa Habari na Uhusiano  wametakiwa kuelimisha jamii kuhusiana na huduma zinatolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) ili kuzijua na kuzitumia ipasavyo.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo Hassan Juma Amour katika mkutano wa Mwaka wa Wadau wa  ZURA uliofanyika huko Ofisini kwao Maisara wa kujadili majukumu ya Mamlaka, mafanikio, changamoto pamoja na mipango yake katika miaka ijayo

Amesema Maafisa Habari na Afisa Uhusiano ndio wadau wakuu wa kutoa na kufikisha taarifa kwa jamii  kwa urahisi pamoja na kuweza kuzitumia huduma na kuibua changamoto  zinazowakabili wananchi na kuzitafutia ufumbuzi  ili kuepukana na athari  zinawowezakujitokeza.

Ameeleza kuwa ZURA inajukumu la kusimamia huduma za maji na nishati zinatolewa kwa uwazi na ufanisi ili kukuza uwekezaji na kuchangia maendeleo ya kiuchumi nchini.

Amefahamisha kuwa ZURA imefanikiwa kuandaa kanuni na miongozo ya Mafuta ,Umeme na Maji ili kumlinda mtumiaji pamoja na kutambulisha utaratibu mpya wa leseni kwa vituo vya Mafuta na Gesi.

 Akielezea changamoto inayoikabili taasisi hiyo ni pamoja na uelewa mdogo juu ya majukumu ya Mamlaka kwa taasisi zinazodhibitiwa na ZURA  pamoja na kuibuliwa kwa maombi mengi ya kuanzishwa kwa vituo vipya vya maji.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.