Kaimu Mkuu wa Tawi la
Utawala Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Hassan
Mabena akitoa taarifa ya kurejeshwa kwa vijana wakujitolea katika mafunzo ya JKT
kuanzia Mei 7 hadi 14, 2021 baada ya kuwarejesha nyumbani hapo awali.
Na Mwandishi wetu-
Dodoma
Mkuu wa Jeshi la
Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Charles Mbuge, amewarejesha katika mafunzo vijana
waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa
kujitolea kwa mwaka 2020/2021 baada ya kurejeshwa nyumbani mwezi Februari 2021.
Akitoa taarifa hiyo
mbele ya waandishi wa habari, Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Kanali Hassan Mabena amesema, vijana hao wanatakiwa kuripoti katika kambi
walizokuwa wamepangiwa awali kuanzia Mei 7 hadi 14. Amefafanua kwamba
vijana waliorejeshwa ni wale wenye elimu ya Darasa la Saba na Kidato cha Nne.
“Vijana wenye Elimu
ya Kidato cha Sita, Ngazi ya Cheti, Stashahada, Shahada na wale wenye Taaluma
ya Uhandisi wataendelea kusubiri majumbani hadi hapo utaratibu mwingine
utakapotangazwa,” alisisitiza Kanali Mabena.
Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT) limekuwa likiendesha mafunzo yakuwajengea uwezo vijana kwa kuwapa stadi za maisha ikiwa ni pamoja na uzalishaji mali, uzalendo, kilimo, ufugaji na kushiriki katika ujenzi wa Taifa.
No comments:
Post a Comment