Habari za Punde

Akinamama wakabidhiwa hati miliki za ardhi Shehia ya Kiungoni, Wete Pemba

BAADHI ya wanawake nane (8) kutoka shehia ya Kiungoni Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, wakisubiri kupatiwa hati miliki za ardhi zao, mradi wa haki ya umiliki wa ardhi Pemba unaoendeshwa na Jumuiya ya KUKHAWA kwa ufadhili wa the Foundation for Civil Society, hafla iliyofanyika katika jengo la MKURABITA kiungoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKURUGENZI wa Jumuiya ya KUKHAWA Pemba Hafidhi Abdi Said, akizungumza wakati wa kikao cha kuwakabidhi hati miliki za ardhi wanawake nane (8) kutoka shehia ya Kiungoni Wilaya ya Wete, hafla iliyofanyika katika jengo la MKURABITA Kiungoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

AFISA Msajili wa ardhi Pemba Yussuf Hamad Kombo, akiwaonyesha wananchi nane (8) wanawake wa kiungoni, jinsi hati miliki za ardhi livyokua na ubora zaidi kufuatia kuwa na picha ya mmiliki wa ardhi husika, hafla iliyofanyika katika jengo la MKURABITA Kiungoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

AFISA Msajili wa ardhi Pemba Yussuf Hamad Kombo, akimjazisha saini mmoja ya wamiliki wa ardhi shehia ya Kiungoni Wilaya ya Wete, ambapo wanawake hao wamepatiwa ardhi zao kupitia Jumuiya ya KUKHAWA Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKURUGENZI wa Jumuiya ya KUKHAWA Pemba Hafidhi Abdi Saidi, akimkabidhi Aziza Abdalla Ismaili mmoja ya wanawake nane wa shehia ya kiungoni ambao wamekabidhiwa hati miliki zao, kwa ufadhili wa Jumuiya ya KUKHAWA Pemba, hafla iliyofanyika katika jengo la MKURABITA Kiungoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)


 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.