Habari za Punde

PBZ Mdhamini Mkuu Ligi Kuu ya Zanzibar. Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar Mpira wa Miguu. Hoteli ya Madinat Al Bahr Mbweni Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla akikabidhiwa mfano wa hundi ya Shs. 346,960,000/=Udhamini wa Ligi Kuu ya Zanzibar na Mkurugenzi Masoko wa PBZ Ndg. Saidi Ali Mwinyigogo hafla hiyo ya Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili ligi Kuu ya Zanzibar umefanyika jana usiku 14-8-2021 katika ukumbi wa Hotel Madinat Al Bahr Mbweni na (kushoto kwa Makamu wa Rais) Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita na Rais wa ZFF Abdul-latif Ali Yassin.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla akikabidhiwa mfano wa hundi ya Shs.346,000,000/= ya Udhamini wa Ligi Kuu ya Zanzibar na CEO wa Azam Media Ltd.Ndg. Yahya Mohammed, hafla hiyo ya Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, umefanyika jana usiku 14-8-2021 katika ukumbi wa Hotel Madinat Al Bahr Mbweni na (kushoto kwa Makamu wa Rais) Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita na Rais wa ZFF Abdul-latif Ali Yassin.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla akikabidhiwa mfano wa hundi ya Shs.50,000,000/= ya Udhamini wa Ligi Kuu ya Zanzibar na Mwakilishi wa  ZMUX Ndg. Omar Abdalla Natepe, hafla hiyo ya Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, umefanyika jana usiku 14-8-2021 katika ukumbi wa Hotel Madinat Al Bahr Mbweni na (kushoto kwa Makamu wa Rais) Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita na Rais wa ZFF Abdul-latif Ali Yassin.
Mkurugenzi wa Masoko wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ltd. Ndg. Said Ali Mwinyigogo akizungumza na kuchangia kwa niaba ya Taasisi yake, wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, uliozinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.
AFISA Muandamizi wa TRZ Ndg. Suleiman Abdalla Said akichangia kwa niaba ya Taasisi yake Shilingi 20,000,000/= , wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, uliozinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.
AFISA wa Mahusiano na Masoko Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Ndg. Mussa Yussuf akizungumza na kuchangia kwa niaba ya Taasisi yake Shilingi 7,000.000/= , wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Udhaminiu na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, uliozinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.
Mkurugenzi Mku wa Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) Ndg. Arafat Ally akizungumza wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar na kuchangia Shilingi 20,000,000/ kwa niaba ya Taasisi yake,wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Udhaminiu na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, uliozinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.
Mchezaji wa Zamani wa Timu ya Small Simba Moto Small Ndg.Omar Hassan Omar King (aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari na Michezo Zanzibar ) akizungumza na kuahidi kuchangia Shilingi 10,000,000/ kwa ajili ya Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Udhaminiu na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, uliozinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.
Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita, akizungumza na kutowa maelezo na madhumuni ya hafla hiyo ya Uzinduzi na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla kuzungumza na Wanamichezo na kufanya uzinduzi wa uchangiaji na ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar kwa mwaka 2021/2022, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar usiku 14-8-2021.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na Wananchezo wa Zanzibar katika hafla ya Uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar  uliofanyika jana usiku katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.
Wachezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa Timu ya Taifa ya Zanzibar  wakimsikiliza mgeni rasmin wa hafla ya uzindudi wa Udhamani na Ufadhili wa ligi Kuu ya Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla (hayupo pichani) akizungumza na wanamichezo wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.
Viongozi wa Vilabu vya Mpira wa Miguuu Zanzibar na Wanamichezo wakifuatilia hutuba ya uzinduzi wa Udhamini na Ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar, wakatin mgeni rasmin Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (hayupo pichani) akihutubia na kuzindua udhamini na ufadhili wa Ligi Kuu ya Zanzibar. hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Al Bahr Mbweni Jijini Zanzibar.



 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.