Habari za Punde

Makamu wa Pili wa Rais, Mhe.Hemed Suleiman Ashiriki Tamasha la Matembezi ya Baskeli Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa kabla ya kuanza rasmi kwa matembeizi ya kutumia usafiri wa Baiskeli yalioanzia Katika Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakili na kumalizia katika eneo la Bustani ya Forodhani.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akiwa pamoja na washiriki wengine katika matembezi ya kutumia usafiri wa baiskeli yalioanzia Katika Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakili kupitia Mji Mkongwe na kumalizia katika eneo la Bustani ya Forodhani.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na washiriki wa matembezi ya usafiri wa baiskeli katika bustani ya Forodhani mapema Leo Asubuhi.


Na.Kassim Abdi

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameyataka mabaraza na Jumuiya za uhifadhi na uwendelezaji Mji Mkongwe kuendelea kutoa Hamasa kwa wakaazi na wageni wanaotembelea Mji huo ili  kujega utamaduni wa kutumia usafiri wa Baiskeli  badala ya vyombo vya moto kwa lengo la kuendelea kuhifadhi mji huo.

Mhe. Hemed alieleza hayo katika mapokezi maalum ya matembezi ya usafiri wa baiskeli yaliyofanyika katika bustani ya Forodhani ambapo yeye binafsi alishiriki kwa kuendesha baiskeli kuanzia ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil na kumalizia katika eneo la bustani ya Forodhani.

Alieleza kuwa, kampeni ya kuhamasisha na kuelimisha jamii juu ya matumizi ya baiskeli  katika eneo la Mji Mkongwe  itasaidia kwa kiasi kikubwa kuhifadhi na kuendeleza  mji huo na kupunguza athari mbali mbali za kimazingira.

Alisema kitendo cha utumiaji wa usafiri wa baiskeli  mbali na kupunguza athari katika mitaa  ya mji huo  wa kale  lakini pia kutasaidia kuimarisha afya za watu ikiwa  utumiaji wa usafiri  wa baiskeli  kuwa sehemu moja wapo ya kufanya mazoezi.

Makamu wa Pili wa Rais alisema katika kukabiliana na changamoto hio Serikali imekuwa ikichukua jitihada mbali mbali za kupunguza uingiaji holela wa vyombo vya moto wa kutunga sheria na kanuni za usafiri zinazodhibiti  uingiaji wa vyombo vya moto pamoja  na kuhamasisha matumizi ya usafiri mbadala.

“Tumekuwa tukihamasisha wananhchi kutumia usafiri  mbadala ikiwemo  matumizi ya usafiri baiskeli ili kukabliana na changamoto ‘’ Alisema Makamu wa Pili wa Rais.

Mhe. Hemed aliendelea kufafanua kwamba, katika kukabiliana na changamoto serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mbali mbali kwa kuweka miundombinu rafiki ya  kuwawezesha wananchi kutembea kwa miguu na kutumia baiskeli  katika mitaa ya Mji Mkongwe.

‘”Sambamba na yote  Serikali imekuwa ikishirikiana na Jumuiya  za kiraia za ndani na nje ya nchi katika  kuhakikisha kuwa tunapunguza matumizi ya vyombo vya moto ili kuunusuru mji wetu  usiendelee kuharibika’’ Alifafanua Mhe. Hemed.

Akimkaribisha Mgeni Rasmi Kaimu Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mhe. Suleiman Masoud Makame  ambae pia ni Waziri wa Maji Nishati na Madini alisema kuna umuhimu mkubwa kwa viongozi kuweka utaratibu maalumu wa kutembea kwa baiskeli ili kutoa hamasa kwa wananchi kutumia usafiri huo.

Aidha, Mhe suleiman alisema kutembea kwa baiskeli katika jiji la Zanzibar ni ishara tosha ya kuwepo kwa amani na utulivu ndani ya Zanzibar, ambapo jambo hilo linawapa fursa wageni kuja kwa  wingi kuitembelea Zanzibar.

Nae Mkurugenzi wa tamasha la Nyama choma ambe pia ni Katibu wa CCM Wilaya ya Mjini Ndugu Abdulrahim Hamid alisema kufanyika kwa matembezi hayo kuna lenga kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais za  kuwinua Mji Mkongwe na kuimarisha utalii kupitia uchumi wa buluu.

Alieleza kuwa, vyombo vya moto vimekuwa vikisababisha athari kubwa kutokana na vishindo vinavyopelekea kuharibika kwa majengo.

Alisema kupitia  kundi hilo la vijana wamekusudia  kufanya tamasha  hilo kuwa endelevu ili kuongeza idadi ya matamasha kwani kufanya hivyo kutapelekea kuongezeka  kwa fursa za ajira kwa vijana .

Mji Mkongwe wa Zanzibar una jumla ya hekta Tisini na sita (96 ) ambapo umekuwa maarufu kwa shughuli za kitalii na ni moja ya miji uliokuwemo katika uhifadhi na urithi wa kimataifa.

Kassim Abdi

Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.

04/09/2021.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.