Habari za Punde

Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan awaapisha Viongozi mbalimbali katika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 13 Septemba, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Makame Mbarawa (Mb) kuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 13 Septemba, 2021.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Januari Yusuf Makamba (Mb) kuwa Waziri wa Nishati katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 13 Septemba, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Dkt. Ashatu Kijaji kuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Dkt. Stergomena Tax kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 13 Septemba, 2021.

Viongozi mbalimbali walioteuliwa Wakila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma katika hafla iliyofanyika katika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 13 Septemba 2021. Kutoka kulia ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa (Mb), Waziri wa Nishati Januari Yusuf Makamba (Mb) Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Tax (Mb), pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali mara baada ya tukio la Uapisho lililofanyika katika viwanja vya Ikulu Chamwino mkoani Dodoma. PICHA NA IKULU



 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.