Na: Lillian Shirima – MAELEZO
Oktoba 14, kila mwaka ni siku ambayo Taifa linaadhimisha kumbukizi ya kifo cha Baba wa Taifa letu na aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mwalimu
Nyerere alifariki dunia Oktoba 14, 1999 katika Hospitali ya Mt.
Thomas iliyopo London, Uingereza alipokuwa
akipatiwa matibabu na kuacha simanzi kubwa ndani na nje ya nchi.
Mzee
Michael Ndesamburo (82) Mkazi wa Kimara mwisho Jijini Dar es Salaam anasema
kwamba sababu kubwa ya kuenzi mchango wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
zinatokana na maono na matendo yake juu
ya taifa la watanzania ambayo ni msingi wa
amani, heshima na utu mwanadamu hadi hii leo.
‘Mwalimu
Nyerere anakumbukwa na kuheshimiwa ndani na nje ya mipaka yaTanzania si
kwasababu alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanzania, hata kidogo, alikuwa kiongozi aliyepigania umoja na utu wa
mwanadamu hata kufanikiwa kujenga taifa lenye amani’. Amesema Mzee Ndesamburo.
Aidha,
amesema Mwalimu Nyerere alikuwa nguzo imara
iliyounganisha taifa la Tanganyika (wakati ule), ambapo alitumia busara
kuliongoza hadi kupata uhuru mwaka 1961 bila kumwaga damu kama mataifa mengine
hatuna budi kuenzi mchango wake.
Akielezea
hali ilivyokuwa wakati wa ukoloni, Mzee Ndesamburo amesema, wakati wa ukoloni watu hawakuishi
kwa kushirikiana bali waliishi kama taifa la mkusanyiko wa watu waliodharauliwa
na kunyanyaswa na utawala wa Mwingereza. Maisha ya jamii yalighubikwa na
mifadhaiko ya utengano pamoja na umasikini.
Wajerumani
walianza kututawala mwaka 1884 hadi 1918 wakifuatiwa na Waingereza mwaka 1918
hadi taifa huru la watu wa Tanganyika lilipoundwa, baada ya kutawaliwa na
wakoloni kwa miaka takriban 77.
‘Ilikuwa
ni mahangaiko na manyanyaso, tulifanya kazi kwenye mashamba ya kahawa kwa ujira mdogo sana, hatukupata faida yoyote sasa hivi mambo
yamekuwa ya kisasa…”. Ameendelea kufafanua Mzee Ndesamburo.
Mzee
Ndesamburo alifika Jijini Dar es Salaam akitokea Tarakea katika Mkoa wa
Kilimanjaro mwanzoni mwa miaka ya 70 akijishughulisha na ushonaji wa viatu na
wakati mwingine akitengeneza saa za mkononi zilizoharibika kwenye eneo la
Posta, (maarufu Posta ya Zamani).
Anasema,
akiwa katika eneo hilo la Posta mara kadhaa anasema alishuhudia msafara wa
Mwalimu Nyerere ukipita katika barabara ya Sokoine (Sokoine Drive) ukitoka au
kuelekea Ikulu na taratibu alijenga mazoea ya kusimama kando barabara hiyo
ambapo Mwalimu alikuwa akiwapungia mkono.
“Nakumbuka nilipata shauku ya kukimbilia
barabara na kumpungia mkono akitoka ikulu, nilijisikia furaha sana kumwona”.
Amemtaja
Mwalimu kama kiongozi aliyeishi maisha ya kawaida, mwadilifu na mzalendo,
aliyetamani kuona watu wakiishi pamoja na kushirikiana katika shughuli za
kimaendeleo.
Licha
ya wingi wa makabila tuliyonayo nchini, Mwalimu
Nyerere atakumbukwa kwa namna alivyoweza kuwaunganisha watanzania katika
lugha moja ya kiswahili iliyoleta
maelewano, kutambuana na kuishi
kama ndugu hali iliyoleta ustawi wa amani
na umoja wa taifa letu hadi hii leo.
Akizungumzia
kuhusu Muungano amesema, Mwalimu alipenda kuona watu wakiishi kwa amani hivyo
kwa kushirikiana na Mwanamapinduzi Shupavu, Mzee Abeid Amani Karume aliyekuwa
Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, waliunganisha Tanganyika na Zanzibar na
kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 26, 1964
‘Sina
wasiwasi tutasheherekea miaka 58 ya Muungano tukiwa na mshikamano imara zaidi
ifikapo Aprili, 2022, sherehe zitafanyika ndani ya taifa salama na utulivu
kutokana na jitihada ziliyofanywa na Mwalimu ambazo viongozi wetu wa awamu
zinaziendeleza”. Anasema Mzee Ndesamburo.
Misingi
ya umoja na mshikamano iliyowekwa na Wazee wetu Mwalimu Julius Nyerere na
Sheikh Abeid Amani Karume imeendelewa kuimarishwa na viongozi wa awamu zote
zilizofuatia kwa upande wa Muungano na Zanzibar na kusababisha utulivu nchini.
Tunamuenzi
Mwalimu kwa utayari wake wa kusaidia mataifa mengine ya Afrika kupata uhuru.
Mwalimu hakuwa mbinafsi, alihimiza watu kuheshimiana bila kujali rika, dini,
kipato, kabila au rangi akiamini kuwa binaadamu wote ni sawa.
Alikuwa
mtetezi wa amani, mlinzi wa rasilimali za taifa, aliyechukizwa na ukabila,
udini, ubadhirifu wa mali ya umma, ulafi wa madaraka , rushwa na uzembe
ulioanza kujitokeza katika ukusanyaji wa kodi.
Katika
hotuba zake hakuacha kukemea dosari zilizojitokeza wakati wa utawala wake na hata baada ya
kung’atuka madarakani. Alisisitiza
ukusanywaji wa kodi kwa maendeleo ya taifa.
Mathalani;
katika hotuma yake ya Maadhimisho ya
Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) iliyofanyika Jijini Mbeya Mwaka
1995, Mwalimu pamoja na mambo mengine
alikemea athari za kutokukusanywa kodi
ambazo zinarudisha nyuma maendeleo ya nchi..
‘…hamkusanyi kodi kwanini? Kwasababu
kutokukusanya kodi mnaviua viwanda vyetu nyumbani hapa…..hata kisingizio cha
kusema ni IMF, ni World Bank si kweli, baadhi yao hao IMF na World Bank ndio wanasema kusanyeni
kodi….kwanini hamkusanyi kodi’. Alisema Mwalimu Nyerere.
Kwa
kuzingatia umuhimu ya ukusanyaji kodi kwa maendeleo ya taifa, Julai, 2020
Tanzania imefanikiwa kuingia kwenye
kundi la nchi za uchumi wa kati ambapo pato la kila Mtanzania limeongezeka hadi
kufikia dola za kimarekani 1,080, ikiwa ni zaidi ya kigezo cha dola za
kimarekani 1,036 cha kuingia kundi hilo.
Mafanikio
haya yamechangizwa na utulivu wa kisiasa, amani na mshikamano katika jamii hali
iliyoruhusu Serikali kuelekeza nguvu kubwa katika kusimamia ukuzaji wa uchumi.
Zimepita
awamu nne (4) tangu Mwalimu Nyerere (Baba wa Taifa) alipong’atuka kwa hiari
madarakani mwaka 1985 na kurudi kijijini kwake Butiama hadi umauti ulipomkuta.
Serikali
ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan iliingia madarakani rasmi Machi 19, 2021 kufuatia kifo cha
aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Pombe Magufuli tarehe 17 Machi,
2021.
Katika
hotuba yake ya kwanza aliyoitoa Bungeni Mjini Dodoma Aprili, 2021, Mhe.
Samia Suluhu Hassan alisema Serikali
yake itaendelea kudumisha mazuri ya awamu zilizopita ikiwa ni pamoja na kulinda
tunu za taifa ambazo ni amani, umoja na mshikamano wa watanzania. TAFUTA NUKUU
“Jambo la kwanza muhimu kabisa tutakalolipa
kipaumbele ni kuendelea kulinda na kudumisha tunu za taifa letu, yaani amani, umoja na mshikamano…….”. Alisema Rais Samia Suluhu Hassan”.
Licha
ya kuendelea kudumisha mshikamano na umoja wa kitaifa, tunaadhimisha miaka 22
ya kifo cha Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere huku Serikali ikiendelea na juhudi za
kuhakikisha maendnchi inazidi kusonga mbele kiuchumi na kijamii.
Moja
ya mikakati wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan aliyoahidi ni kuimarisha mazingira bora ya uwekezaji nchini
yatakayovutia uwekezaji zaidi pamoja na ukusanyaji kodi ya Serikali.
Kwa
kipindi kifupi toka aingie madarakani, miradi ya uwekezaji imeongezeka na
kufikia dola bilioni 3.5 mwaka huu
ukilinganisha na dola milioni 647 katika kipindi cha mwaja jana.
Mbali
na mafanikio hayo. taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO
ambaye ni Msemaji wa Serikali Mkuu wa
Serikali Gerson Msigwa Oktoba 2, 2021,
ilionesha ukusanyaji wa mapato kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
umeongezeka ikilinganishwa na mwaka 2020 ambapo zilikusanywa Shilingi Trilioni
1 na Bilioni 703 sawa na asilimia 80 ya malengo ya kukusanya Shilingi Trilioni
2 na Bilioni 229.
Makusanyo
ya mwezi Septemba, 2021 ni Shilingi Trilioni 1 na Bilioni 970 sawa na asilimia
93 ya malengo ya kukusanya Shilingi Trilioni 2 na Bilioni 128.
Serikali
ya Awamu ya Sita imeongeza kasi
kuhakikisha miradi yote ya kimkakati iliyoanzishwa kama vile Ujenzi wa
Bwawa la Kuzalisha Umeme Mto Rufiji (JNHPP), Reli ya Kisasa (SGR), Barabara na
mingine mingi inakamilika kama ilivyopangwa kwakuwa lengo ni kuleta maendeleo
kwa wananchi.
Tuenzi
mchango wa Mwalimu Nyerere Kiongozi aliyekuwa na juhudi za kutimiza ndoto za
watanzania akiamini kwamba tunu za umoja na amani tulizojaliwa na Mwenyezi
Mungu ni msingi wa malezi ya taifa huru katika kuleta maendeleo ya watu wake.
Pumzika
kwa amani, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere, Tanzania ipo imara.
MWISHO.
Kwa
upande wa huduma ya afya kazi kubwa iliyofanywa tangu 2015 mpaka sasa.
Tumefanikiwa kuongeza idadi ya hospitali kutoka ..zilizokuwapo wakati tunapata
uhuru hadi kufikia hospitali ……hivi sasa. Zahanati nazo zimeongezeka kutoka
…..mwaka 1961 hadi 4,679 hivi leo. Tumeongeza pia idadi ya vituo vya afya
vijijini kutoka vituo 22 tulivyorithi kutoka kwa wakoloni hadi vituo 481 vya
sasa. Watu wengi zaidi sasa wanapata huduma ya afya kuliko ilivyokuwa wakati wa
ukoloni. Afya za Watanzania wengi zimeimarika zaidi sasa kuliko ilivyokuwa.
Watu sasa wanaishi miaka mingi zaidi na ndiyo maana idadi ya watu ni mara….ya
wale waliokuwepo wakati nchi yetu inapata uhuru.
Bado tunayo kazi kubwa ya kuboresha huduma ya
afya nchini kwa kujenga zahanati na vituo vya afya na hospitali zaidi.
Kuboresha huduma ya watoto na mama wajawazito na kupambana na maradhi yanayoua
watu wengi kama vile malaria, ukimwi, kifua kikuu na mengineyo.
Tangu
tupate uhuru Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kupanua huduma za
usafiri wa barabara, reli, anga na usafiri wa majini. Tumepata mafanikio
makubwa na ya kutia moyo. Maeneo mengi vijijini sasa yanafikika kwa barabara.
Bila
miundombinu bora uchumi wetu hauwezi kukua haraka. Pia panapokuwepo na barabara
watu hutumia magari badala ya kutembea kwa miguu, hivyo kufanya maisha kuwa
rahisi na bora zaidi.
Aidha,
Serikali itaendelea kujenga mazingira mazuri ya kiuchumi na kibiashara ili
kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza zaidi nchini mwetu. Pia
tutahakikisha kuwa vikwazo vinavyokwamisha uanzishaji na uendeshaji biashara
hapa nchini vinaondolewa mapema ili kuimarisha sekta ya biashara na uwekezaji
ambayo ni muhimu sana katika kuleta ajira nchiniSerikali itaendelea na kazi ya
kukamilisha programu ya uwekezaji katika sekta utalii miundombinu ili
kurahisisha mawasiliano na hivyo kuchochea kukua kwa shughuli za kiuchumi na
kibiashara hapa nchini.
Reli
ya TRC na TAZARA na viwanja vya ndege pamoja na kuviimarisha na kuboresha
vilivyopo
kila mmoja wetu afanye kazi kwa bidii na maarifa ili kwa pamoja tusukume mbele gurudumu la maendeleo ya nchi yetu. Jambo hili linawezekana ikiwa sote tutadhamiria hivyo. Tukumbuke msemo maarufu wa muasisi wa taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere usemao………………….
Kwa upande wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii nayo tumepata mafanikio makubwa. Hali ya maisha ya Watanzania ilivyo leo sivyo ilivyokuwa wakati Mwalimu anang’tuka madarakani 1985
Wakati tunapata uhuru hali ya upatikanaji wa
elimu nchini ilikuwa ni duni sana. Sehemu ndogo sana ya watu wetu waliweza
kupata elimu. Hivyo, watu wengi walikuwa wanakabiliwa na tatizo la ujinga.
Mwalimu Nyerere aliutangaza ujinga kuwa moja ya
maadui watatu wa nchi yetu pamoja na umaskini na maradhi. Hali ilikuwa hivyo
kwa sababu ya ufinyu wa fursa za kupata elimu hasa kwa Waafrika. Kwa sababu ya
ubaguzi Serikali ya ukoloni haikujali na hivyo haikujihusisha vya kutosha na
elimu kwa wananchi.
Kazi hiyo iliachiwa mamlaka za wenyeji na mashirika ya dini na hasa makanisa kuifanya pale ambapo yalipobahatika kuwepo. Hata pale Serikali ilipojihusisha ilijali zaidi elimu ya kupata makarani tu na siyo kupata watu wenye taaluma muhimu kwa maendeleo kama vile udaktari, uhandisi na kadhalika. Kwa jumla, wakoloni walikuwa na sera ya makusudi ya kutokuwasomesha Waswahili ili wawatawale vizuri.
No comments:
Post a Comment