Habari za Punde

MAKAMU WA RAIS AKIONDOKA KUELEKEA MALAWI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Philip Mpango akiagana na viongozi mbalimbali katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam wakati akiondoka nchini kuelekea Lilongwe nchini Malawi kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi wananchama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 12 Januari 2022. 


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Philip Mpango hii leo tarehe 10 Januari 2022 anaondoka nchini kuelekea Lilongwe nchini Malawi kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi wananchama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 12 Januari 2022.

Mkutano huo utatanguliwa na Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa , Ulinzi na Usalama (Organ Troika Summit) utakaofanyika tarehe 11 Januari 2022.

Franco Singaile

MMR – Habari. Januari 10,2022.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.