Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi amehudhuria maziko ya mama mzazi Makamu wa Rais Mstaaf wa Tanzania Alhaj.Dkt. Mohammed Gharib Bilal

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar,Sheikh Saleh Omar Kabi, baada ya kumalizika kwa Sala ya kuusalia mwili wa Marehemu Safia Abeid Mama Mzazi wa Makamu wa Rais Mstaaf wa Tanzania Alhaj.Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kushoto kwa Rais) iliofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Wilaya ya Mjini Unguja, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla na Rais Mstaaf wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein ( kulia kwa Rais) Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhaj Othman Masoud Othman, Rais Mstaaf wa Zanzibar Alhaj.Dkt.Amani Karume na Makamu wa Pili Mstaaf Alhaj Balozi Seif Ali Iddi.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi katika maziko ya Marehemu Safia Abeid Mama Mzazi wa Makamu wa Rais Mstaaf wa Tanzania Alhaj Dkt. Mohammed Bilal,Mtoto wa Marehemu Bw. Abeid, Makamu wa Pili wa Rais Mstaaf Alhaj Balozi Seif Ali Iddi,yaliyofanyika katika Kijiji cha Kiboje Wilaya ya Kati Unguja na (kulia kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Rashid Hadidi Rashid.(Picha na Ikulu)
MAKAMU wa Rais Mstaaf wa Tanzania Alhaj.Dkt.Mohammed Gharib Bilal akiweka mchanga katika kaburi la Mama Yake Mzazi Marehemu Bi.Safia Abeid,baada ya kuweka mwili wa marehemu maziko yaliyofanyika Kijiji kwao Kiboje Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo 4-1-2022.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiweka mchanga katika kaburi la Marehemu Bi.Safia Abeid, Mama mzazi wa Makamu wa Rais Mstaaf wa Tanzania Alhaj Dkt.Mohammed Gharib Bilal, maziko yaliofanyika Kijiji kwao Kiboje Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akitowa mkono wa pole kwa Makamu wa Rais Mstaaf wa Tanzania Alhaj Dkt.Mohammed Gharib Bilal, kwa kufiwa na Mama yake mzazi marehemu Safia Abeid, baada ya kumalizika kwa maziko hayo yaliyofanyika katika kijiji cha Kiboje Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.(Picha na Ikulu)

STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

 Zanzibar                                                                                               04.01.2022

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi leo ameshiriki mazishi ya Marehemu Bi Safia Abeid, mama mzazi wa Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal yaliyofanyika huko kijijini kwao Kiboje Mwembeshauri, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.

Viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa, dini na Serikali, wananchi pamoja na wanafamilia walihudhuria katika mazishi hayo ambapo mapema Alhaj Dk. Mwinyi aliungana nao katika sala ya kumuombea Marehemu iliyosaliwa huko  Masjid Jaami Zinjbaar, Mazizini, Jijini Zanzibar.

Imetayarishwa na Kitengo cha Habari.

Ikulu Zanzibar.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.