Habari za Punde

Matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia bado ni tatizo kwa jamii

 Na Mwashungi Tahir        Maelezo 

 Jumla ya matukio 65 ya ukatili na udhalilishaji wa jinsia yameripotiwa mwezi wa January ,2022 ambapo wengi wao walikuwa ni watoto ambao ni asilimia 75.4 na wanawake ni asilimia 24.8. 

Akiwasilisha  Takwimu  za ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto kwa mwezi wa January 2022 Mtakwimu kutoka kitengo cha makosa ya jinai na jinsia  katika ofisi  ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali  Asha Mussa Mahfoudh wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko katika ukumbi wa Mtakwimu Mkuu uliopo Mazizini .

Amesema mlinganisho kwa idadi ya matukio kwa mwezi wa Januari  imepungua kwa asilimia 13.0 kutoka matukio 97 kwa mwezi wa Disemba 2021 hadi 65  mwezi wa Januaty 2022.

Akitoa taarifa za Wilaya amesema Wilaya ya Magharibi “B” imeripotiwa kuwa na matukio mengi ukilinganisha na Wilaya nyengine matukio 13 zikifuatiwa na Wilaya ya Wete matukio 11 , na Wilaya ya Magharibi “A” matukio 10.;

Kwa Wilaya ya Kaskazini “B” muwasilishaji Asha  amesema imeripotiwa kuwa na idadi ndogo ya matukio kuliko wilaya zote tukio moja 1 na wilaya ya Mkoani hakuna tukio lililoripotiwa.

Amesema matukio 54 kati ya matukio 65 yaliyoripotiwa yapo chini ya upelelezi wa Polisi, na matukio 11 yapo hatua nyengine ambapo matukio sita yapo Ofisi ya Mashtaka na matukio 5 yapo mahakamani.

Nae Mratibu  msaidizi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi mkuu wa kitengo cha Takwimu za makosa ya jinai Ramadhani Himid amewataka wazazi kuwa  karibu na watoto wao kwani vitendo hivyo  hutokea sana maskuli au madrasa na kutoa tahadhari kwa wageni wasiaminiwe kabisa wanapofika mitaani.

Pia Mwenyekiti wa Mahkama  ya watoto Zuweina Mohammed Abdullah amesema jamii  iwe karibu na watoto kwa kuwapa elimu ili waepukane na vitendo vya udhalilishaji hasa kulawiti.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Bodi Amina Salum Ali amefanya uzinduzi wa  kitabu cha Ripoti  cha viashiria vya jinsia vilivyomo katika mpango wa maendeleo endelevu (EDGS) Zanzibar.

Akitoa wito baada ya uzinduzi huo mwenyekiti huyo amesema nguvu zizidishwe kwa kuwalinda watoto na kuwaacha kwa muda mrefu bila kujua wako wapi na wanacheza na watu wa aina gani.

Pia ameomba sheria ya watoto ipitiwe upya kwa lengo la kuwarekebisha watoto   kupatiwa adhabu iliyokuwa ngumu kidogo ili  waweze kujirekebisha  na waache kufanya vitendo hivyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.