Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Ameongoza Mamia ya Wananchi wa Kijiji cha Nyasusura Katika Maziko ya Mlinzi Wake Marehemu Kagere.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Mkoa baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Mwanza akielekea Mkoani Mara kuhudhuria maziko ya mlinzi wake Marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro aliyefariki wiki hii.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimfariji na kumpa mkono wa pole Mama Mzazi wa Marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro.Bi. Grace Mukakaro, baada ya kuwasili katika Kijiji cha Nyasusura Mkoani Mara kuhudhuria maziko hayo yaliofanyika leo 26-2-2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiwafariji Watoto na familia  ya Marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro, baada ya kuwasili Kijijini kwao Nyasusura Mkoani Mara, kuhudhuria maziko hayo yaliofanyika leo
VIJANA walioandaliwa kwa ajili ya kuchukua jeneza likiwa na mwili wa Marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro wakiwasili katika eneo lililotengwa kwa ajili ya maziko kijiji kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakijumuika na Viongozi wa Serikali na Wananchi wa Kijiji cha Nyasusura Mkoani Mara katika maziko ya marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro yaliofanyika leo 26-2-2022, kijiji kwao.
WANAFAMILIA ya Marehemu Kagere wakiongozwa na Mama Mzazi wa Marehemi Bi Grace Mukakaro (mwenye gauni jeupe) akiwa na Watoto wa marehemu na Mjane wa Marehemu Bi. Gladyness Tandila wa mwinsho (mwenye gauni jeusi) 
WANAFAMILIA ya Marehemu Kagere wakishirika katika ibada maalum ya kumuombea wakati wa maziko hayo yaliofanyika kijijini kwao nyasusura Mkoani Mara leo 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akitowa salamu za pole kwa Wanafamilia na Ndugu wa Marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro aliyekuwa mlinzi wake, wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijiji kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022
WANANCHI wa Kijiji cha Nyasusura Mkoani Mara wakishiriki katika Ibada maalum ya kumuombea marehemu wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijiji kwao leo 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakitowa heshima za mwisho kwa Marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro aliyekuwa mlinzi wake, wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijiji kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022


MAMA Mzazi wa Marehemu Kagere Bi Grace Mikakaro akitowa heshima ya mwisho kwa marehemu wakati wa maziko yaliofanyika Kijijini kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022.
MJANE wa Marehemu Kagere Bi. Gladeness Tandila akitowa heshima ya mwisho kwa marehemu mume wake Kagere wakati wa maziko yaliofanyika kijijini kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022, akisaidiwa na ndugu na jamaa
WATOTO wa Marehemu na Ndugu na Jamaa wakitowa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kagere wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijiji kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022

WANANDUGU wa Marehemu Kagere wakiongozwa na Mama Mzazi wa Marehemi Bi. Grace Mukakaro akiwa na Mjane wa Marehemu Bi. Gladeness Tandila na Mtoto wa marehemu wakiweka mchanga katika kaburi baada ya kuwekwa mwili wa marehemu wakati wa maziko hayo yaliofanyika kijijini kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022
WATOTO wa Marehemu Kagere wakiweka mchanga katika kaburi la baba yao wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijijini kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiweka mchanga katika kaburi la aliyekuwa mlinzi wake marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro, yaliofanyika Kijijini kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiweka shada la maua katika kaburi la marehemu Kagere Thomas Charles Mukakaro, aliyekuwa mlinzi wake, baada ya kuwekwa mwili wa marehemu wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijiji kwao Nyasusura Mkoani Mara leo 26-2-2022.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.