Habari za Punde

Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar Ndg.Shaib Ibrahim Mohammed akitembelea shamba la Vijana la mbongamboga Wilaya ya Kati Unguja, akiwa katika ziara yake kutembelea vikundi vya Vijana Mkoa wa Kusini Unguja.

Na.Mwandishi Wewtu.

MKURUGENZI Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar  Shaib Ibrahim Mohamed alisema Serikali kwa kushirikiana na shirika la umeme ZECO itahakikisha kuwatengenezea mazingira bora  ambayo yatawawezesha vijana  ili kujipatia kipato.

 Ameyaeleza hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea wadau na vikundi mbali mbali vinavyojishughulisha katika masuala ya kilimo pamoja  na uwezeshaji wa vijana huko Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Alisema pamoja na changamoto za miundombinu ya maji na umeme  lakini bado  hawajakata tamaa kwani serikali inachukua jitihada na kuahidiwa kupelekewa  huduma hizo

Aliwapongeza vijana kwa kubuni shughuli   za kilimo ,ufugaji wa samaki  katika kujiletea maendeelo ambapo  serikali inaendelea kuwaunga mkono ili vijana kujikwamua na hali ya umasikini.

Akizungumzia kuhusu mradi wa pesheni alisema vijana wamepiga hatua na kuweza kuzalisha na wamekuwa na mwamko wa kuwapatia  taaluma  vijana wengine jinsi ya kuzalisha mapesheni hayo.

Katibu wa kikundi cha ushirika umbuji famili Abdulghani Choum Khamis alisema wameamua kufanya shughuli za kilimo kwa lengo la kujikwamua kimaisha na kusaidia familia zao katika masuala ya elimu.

Katika ziara hiyo maeneo yaliyotembelewa ikiwemo kikundi cha ushirika Koani,  Chuo cha maendeleo Dunga kikundi cha ushirika Bambi, Pagali,kikundi cha ushirika Umbuji famili, pamoja na Dunga kibweni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.