Habari za Punde

Waziri Mhe. Masoud Amewata Mafundi Kuwa Wazalendo Kuzingatia Viwango Kupata Majengo Yenye Ubora.

Na Rahma Khamis Maelezo    Zanzibar.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe, Masoud Ali Mohammed amewataka mafundi kuwa wazalendo katika ujenzi kwa kuzingatia viwango ili kupata majengo yenye ubora nchini.

Akiwa katika ziara ya  kukagua majengo ya kikosi cha Valantia amesema amefurahishwa na kasi ya ujenzi huo kuona unaenda vizuri ambao unajumuisha   nyumba za wakuu wa kambi, ofisi, mahanga ya wapiganaji  pamoja na  nyumba za kuishi wapiganaji wa kikosi hicho.

Amesema kuwa ili majengo yawe imara  lazima kuzingatia  ubora wa vifa vya ujenzi pamoja na kujali muda uliyopangiwa kukamilika hivyo  kasi ya ujenzi huo inatarajiwa   kukamilika kwa muda mfupi.

Aidha amefahamisha kuwa ingawa jengo linalojengwa katika eneo la kikungwi litakua na nyumba ya Mkuu wa wa Kambi hiyo ,pia litakuwa na makao makuu ya kambi  ili wapiganaji waweze kuishi.

Waziri ameongeza kusema kuwa licha ya kuwepo kwa majengo ya ofisi pia wapiganaji wana haki ya kujenga  kila wanachohisi muhimu kujengwa katika eneo hilo ili kurahisisha huduma muhimu zinazohitajika.

Aidha Waziri huyo amemtaka Enginear anaesimsmamia ujenzi huo kuhakikisha ujenzi unakuwa na kiwango na kukamilika kwa wakati.

Nae Mkuu wa Kikosi cha Valantia Luten Kanal Saidi Ali Shamhuna amesema vifaa vyote vya ujenzi vipo hivyo  wanaendelea kujenga na kuhakiksha kuwa ujenzi huo.

Ziara hiyo imejumuisha kutembelea maeneo mbalimbali ikiwemo Muyuni C’Kikungwi, Mto wa maji na Mwanyanya ambapo katika eneo hilo wameomba kupatiwa barabara. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.