Habari za Punde

Kuwapatia Elimu Watoto ni Jukumu la Wazazi Kwa Kushirikiana na Wadau Mbalimbali wa Elimu.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dkt Mwanakhamis Adam  Ameir amesema suala la kuwapatia elimu watoto ni jukumu la wazazi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Elimu ili taifa liweze  kupata wataalum wa baadae.

Akifungua mkutano wa kupanga mikakati ya kuwasaidia watoto kurudi Skuli kwa Polisi jamii wa Wilaya ya Magharibi B katika ukumbi wa Aboud Jumbe Mwinyi huko fuoni Mkoa wa Mjini Magharib Unguja amesema elimu ni haki ya msingi ya kila mtoto hivyo wazazi nao wanapaswa  kuwasimamia ili kuipata haki hiyo.

Amesema Wizara ya Elimu kupitia mradi wa kuwarejesha watoto Skuli walio na umri wa miaka Saba Hadi 14 watahakikisha  wanatumia mikakati madhbuti ili watoto hao wafanikishe ndoto za maisha yao.

Aidha  Dkt Mwanakhamis amewaomba Polisi Jamii hayo kupanga mikakati  itakayosaidia kuapatina watoto hao katika maeneo yote ya shehia zao.

Kwa upande wake mkurugenzi idara ya Elimu mbadala na watu wazima bi mashavu Ahmada fakih amesema kwa hatua ya awali Wizara kwa  kushirikiana na jamii kupituia mradi huo  tayar  wameweza kurejesha zaidi ya Wanafunzi  elfu10 hivyo Bado jitihada zinahitajika ili kuliondosha kabisa tatizo ilo Katika jamii zao.

Nae Mratibu wa Mradi wakuwarejesha watoto Skuli Bw Mzee Shiraz Hassan amesema katika kuwahamasisha watoto kurudi Skuli na kubaki madarasani ni pamoja na kuwapatia sare za Skuli na vifaa vya kujifundishia kwa lengo la kuwapa hamasa ya kuendelea na masomo.

Kwa upande wao Polisi Jamii hao wamesema ili kuwasaidia na kuwaondosha wimbi la watoto walioacha masomo katika mikakati yao ni kuondoshwa michezo ya  gemu katika mitaa ambazo zinachangia kuwepo kwa wimbi kubwa la  watoto watoro.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.