Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Amefunga Mkutano wa Wadau wa Demekrasia ya Vyama Vingi vya Siasa Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Zanzibar

Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akisoma hotuba ya Ufungaji wa Mkutano wa Siku tatu wa Mkutano wa wadau wa Demokrasia  uliofanyiaka hoteli ya Golden Tulip Zanzibar kwa ajili ya kujadili mambo makhusi ya Zanzibar yanayohusu Vyama Vingi vya Siasa.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Msoud Othman, amesema Dunia imekuwa ikishuhudia mabadiliko makubwa ya kiuchumi , Kisiasa na Kijamii na ya Teknlolojia  na kwamba  nchi haiwezi kuyaepuka kwa kuwa ndio yanayoakisi siasa za Ulimwengu na Tanzania kwa jumla.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege mjini Zanzibar alipofunga mkutano wa Wadau wa Demokrasia uliojadili masuala makhususi ya Zanzibar  yanayohusu Vyama vingi vya Siasa.

Mhe. Makamu amesema kwamba  siasa za dunia ya sasa ni ushindani , ubunifu na ufanisi na iwapo nchi itashindwa katika masuala hayo inaweza kuwa ni msindikizaji na hivyo ni vyema kuicha historia ya kisiasa nchini kuwa mwalimu, lakini sio izuie nchi kusonga mbele.

Aidha Mhe. Othman amewaeleza  washiriki hao kwamba kuna umuhimu kama taifa kujiuliza sababu za mageuzi yanayohitajika ndani ya nchi na kukubalika na wananchi  na kwamba mtazamo wa kimageuzi lazima ufanane kifikra kwa wananchi  wote ili kuweza kufikia mageuzi ya kweli ya kidemokrasia.

Amefahamisha kwamba maegeuzi ni muhimu kufanyika  katika ustawi wa kiuchumi hasa kwa vile Zanzibar inategemea sana biashara ya huduma na bidhaa,  lakini kwa kutegemea uwekezaji wa fedha nyingi sambamba na utaalamu wa hali ya juu ili kuvutia uwekezaji utakaoleta mabadiliko ya kweli ya kiuchumi na  kijamii chini ya kivutio cha amani endelevu nchini.

Aidha amesema kwamba kivutio cha pili kikubwa cha mageuzi ni sera bora, ni kuwepo taasisi madhubuti na mifumo ya kisasa ya kiserikali ya kuhudumia biashara na uchumi.

Mhe. Othman ameongeza kwamba kivutio cha tatu ni uwezo wa nchi katika kushindana na ufanisi wa wengine na kwamba malengo ya mageuzi hayo ni lazima yawe na maono mapana zaidi wa  siasa na ushindani wa kiitikadi.

Amesema kwamba hali hiyo itasaidfia kuhakikisha kuwepo mageuzi ya kujenga Zanzibar mpya,  itakayosimama  pahala inapostahiki kwa kuwa mafanikio ya nchi kama vile Mauritius ambayo ni ndogo  kuliko Zanzibar lazima yaifikirishe Zanzibar  pahala pa mafanikio hasa kwa vile ina mazingira bora ya kuweza kufika mbali kimaendeleo.

Mhe. Makamu amesema katika utekelezaji wa kweli wa demokrasia na ulazima wa mageuzi ya kujenga Zanzibar mpya kuna haja ya kuwa na chombo makhusi cha kusimamia maridhiano na demokrasia nchini.

Mhe. Amewataka Wazanzibari wote wakiwa ni wazazi na viongozi  wanawajibu wa kuwarithisha nchi iliyotayarishwa kuendana na dunia ya sasa, yenye amani ya kweli, yenye utulivu, mshikamano na mifumo itakayowapeleka mbele na kwamba Zanzibar hainachaguo katika hilo.

Mhe. Othman amefafanuya kuwa Ili  Zanzibar na Tanzania kwa jumla kutekeleza Dira hiyo,  kunahitajika kuwepo ukweli, katika kauli na matendo  kwa viongozi ili ile dhamira aliyokusudiwa  ya kujenga Zanzibar mpya iweze kufanikiwa .

Amewataka wazanzibar na watanzania kwa jumla kuelewa  kwamba dhamira ya kujenga umoja na Amani ya kweli nchini haipaswi kutikiswa wala kuyumbishwa na changamoto za ndani au nje ya mirengo ya siasa na  kiitikadi na kufikiria sana umuhimu wa kuvumiliana. 

Mhe. Othman amewataka wanaanchi na Viongozi wa kisiasa kufahamu kwamba ni lazima kuamini  viongozi  wanaweza kujenga misingi ya kuendesha nchi yao kwa misingi inayoakisi maendeleo ya dunia ya leo.

Hata hivyo, amesema kwamba katika kujenga demokrsia ya kweli na Zanzibar mpya ni vyema, pamoja na hadhari ya kutotonesha vidonda, lakini vipatiwe dawa ili  vidonda hivyo vibaki kuwa kovu.

Naye waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais , sera,  Uratibu na Baraza la Wawakilishi Mhe. Hamza Hassan Juma,amesema mkutano huo ulikuwa na mafanikio makubwa na kwamba washiriki walipata fursa ya kujadili kwa uwazi mada mbali mbali zilizowasilishwa.

Amefahamisha kwamba mada hizo zilikuwa ni chimbuko la mjadala na washiriki kuelewa vitu vingi na kwamba ni busara wanasiasa kurudi kwa wananchama kuelezea nia ya dhati ya viongozi wakuu ya kutaka kujenga Zanzibar na Tanzania mpya katika mustakabali wa maendeleo endelevu.

Amesema kwamba katika masuala ya kujenga Amani, viongozi wa dini wamekuwa na mchango mkubwa na kuiyomba serikali kuwashirikisha zaidi ili waweze kutoa mchango zaidi katika maendeleo ya nchi hasa katika kustawisha amani.

Amewataka wanasiasa na Viongozi kunga mkono maono na nia njema ya rais Mwinyi katika kuetekeleza nia ya dhati ya kujenga taswira ya kila mmoja kushiriki katika maendeleo ya Zanzibar katika kujenga Zanzibar mpya.

Mkutano huo wa Wadau  wa Demokrasia  kujadili masuala makhusuri ya Zanzibar yanayohusu vyama vingi vya Siasa umeitishwa kufuatia agizo la Rais Mwinyi Kutaka kujadiliwa masuala hayo kutokana na umuhimu wa kipekee kwa Zanzibar

Imetolewa leo na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Kupitia Kitengo cha habari leo tarehe.6/10/2022.

Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya sisasa walioshiriki katika Mkutano wa wadau wa Demokrasia  uliofanyiaka hoteli ya Golden Tulip Zanzibar kwa ajili ya kujadili mambo makhusi ya Zanzibar yanayohusu Vyama Vingi vya Siasa  wakifuatilia houtuba ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, alipokuwa akifunga mukutano huo 
Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya sisasa walioshiriki katika Mkutano wa wadau wa Demokrasia  uliofanyiaka hoteli ya Golden Tulip Zanzibar kwa ajili ya kujadili mambo makhusi ya Zanzibar yanayohusu Vyama Vingi vya Siasa  wakifuatilia houtuba ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, alipokuwa akifunga mukutano huo 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.