Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mary Masanja (Mb), ameziagiza taasisi za Wizara yake kutenga nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) kila mwaka ili kuendana na kasi ya ongezeko la wanafunzi na kuchangia upatikanaji wa maeneo ya mafunzo kwa vitendo sambamba na kutoa ajira kwa wanafunzi hao pale nafasi zinapopatikana.
Ameyasema
hayo katika mahafali ya ya 20 ya Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) yaliyofanyika
katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere (JNCC) jijini Dar
es Salaam.
Amesema
kuwa maendeleo ya utalii kitaifa yataweza kufikiwa endapo wadau wote
watashiriki katika jitihada za kuelimisha, kuendeleza, kukuza na kuitangaza
Tanzania na kwamba kwa kuboresha huduma bora za utalii kutaongeza tija katika
sekta hiyo.
“Hatuna
budi kuhakikisha kuwa huduma mbalimbali za utalii zinazotolewa zinabeba weledi
unaostahili. Weledi huu utaonekana vizuri zaidi katika huduma zetu endapo
tutaajiri wataalam wenye ujuzi stahiki kama wanaohitimu leo hii” Mhe. Masanja
amesema.
Aidha,
ametoa rai kwa wadau wa sekta ya utalii nchini kuhakikisha kuwa huduma
mbalimbali za utalii zinazotolewa zinabeba weledi unaostahili na kwamba hilo
litaonekana vizuri zaidi kwa vitendo endapo wataajiri wataalam wenye ujuzi
stahiki kama wanaohitimu katika chuo hicho.
“Ifike
mahali nchi yetu tujivunie kutoa wataalam wanaotosheleza soko la ndani na
kupata fursa ya kutoa huduma katika soko la nje kama ilivyo kwa jirani zetu”
amesema.
Sambamba
na hilo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia
Suluhu Hassan kwa kufanya jitihada za kuhakikisha utalii unaimarika ikiwemo
uzinduzi wa Royal Tour ambayo imeleta hamasa kubwa kwa wageni na wenyeji.
Kwa
upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Utalii (NCT), Dkt. Florian Mtey, amewataka
wahitimu hao kuzingatia sheria, taratibu, kanuni na miongozo iliyopo ya
utumishi wa umma wakatapokuwa wakitimiza majukumu yao wakiwa kazini.
Mahafali
hayo yamehudhuriwa na Mabalozi, Wakuu wa Taasisi mbalimbali,Wadau wa Sekta ya
Utalii na Ukarimu, Watumishi na Wanachuo,
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe. Mary Masanja (Mb) (wa pili kutoka kulia)akiwa katika maandamano ya mahafali ya 20 ya Chuo Cha Taifa cha Utalii (NCT) jijini Dar es Salaam. Wengine ni menejimenti ya Chuo Cha NCT.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja (Mb) (kulia) akionyesha zawadi ya picha aliyokabidhiwa na mwanafunziwa wa Chuo cha Taifa cha Utalii katika kozi ya Basic Technician Certificate in Event Management Glory Siame wakati wa mahafali ya 20 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment