Habari za Punde

TanTrade yaandaa mafunzo ya utumiaji wa Mifumo ya Biashara Zanzibar kwa viongozi wa umma na Taasisi Binafsi

Waziri wa Biashara na Maenedeleo ya Viwanda Zanzibar Omar  Said Shaaban akifunguwa mafunzo ya Viongozi wa umma na taasisi binafsi ya utumiaji mifumo ya Biashara Zanzibar  huko Afisi ya ukumbi wa Zura Maisar (kulia) Makamo Mwenyekiti wa bodi ya biashara Zanzibar Tran trade Dkt. Issa Seif Salim (kushoto) Naibu Katibu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda  Rashid Ali Salim.
Mwenyekiti wa bodi ya biashara Zanzibar Tran trade Dkt. Issa Seif Salim  akitoa taarifa Viongozi wa umma na taasisi binafsi kuhusu mafunzo ya utumiaji wa mifumo ya Biashara Zanzibar  huko Afisi ya ukumbi wa Zura Maisara
 Naibu Katibu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda  Rashid Ali Salim akitowa maelezo kwa  Viongozi wa umma na taasisi binafsi waliofika katika mafunzo yaliyandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TAN  TRADE) yaliyofanyika huko ukumbi wa Afisi ya Zura Maisara. (Kushoto) Waziri wa Biashara na Maenedeleo ya Viwanda Zanzibar Omar  Saaid Shaaban na Mkurugenzi wa huduma za Biashara Tan Trade Twilumba Mlelwa.
Mshauri Mfumo wa Biashara Tan Trade  Gema Mwikoko akitoa mafunzo kwa Viongozi wa umma na taasisi binafsi  walifika katika ukumbi wa Afisi ya Zura Maisara mjini Zanzibar.

 Baadhi ya washiriki wakimsikiliza mkufunzi Gema Mwikoko( hayupo pichani) wakati akitowa mafunzo kuhusu  mada mfumo wa taratibu za biashara yaliyofanyika Afisi ya ukumbi wa Maisara Mjini Zanzibar.

Picha na Miza Othman- Maelezo Zanzibar.

Na Khadija Khamis – Maelezo Zanzibar, 14/12/2022.

Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Omar Said Shaaban  amesema utumiaji wa mifumo ya biashara utasaidia kukuza biashara na kurahisisha upatikanaji  wa  masoko ya bidhaa  ndani na nje ya Nchi .

Ameyasema hayo katika ukumbi wa ZURA, Maisara wakati akifungua mafunzo ya utumiaji wa Mifumo ya Biashara Zanzibar kwa viongozi wa umma na Taasisi  Binafsi zinazohusiana na biashara.

Amesema hatua hiyo ni kubwa katika kutimiza azma ya Serikali  ya kuhakikisha inakwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia ya Dunia kwa kufuata mfumo wa kibiashara ili  kurahisisha kukuza biashara pamoja na kupata masoko kwa urahisi ya ndani na nje ya nchi .

Aidha alisema mfumo huo utasaidia kupata taarifa mbali mbali ikiwemo za masoko ya biashara za kimataifa kupata vibali, leseni na kujua vigezo vya biashara pamoja na kufanya maamuzi sahihi ya nchi ambazo zinatoa bidhaa bora.

Waziri huyo aliwataka viongozi hao kusimamia mfumo huo na kuwaeleza wafanyabiashara jinsi ya  mwenendo wa soko duniani pamoja na kushuka na  kupanda kwa bei za bidhaa.

Nae Naibu Katibu Mkuu  wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Rashid Ali Salim amesema mfumo wa uwezeshaji biashara zinasimamiwa na mamlaka ya maendeleo ya biashara Tanzania TanTrade .

Alifahamisha kuwa TanTrade ni chombo cha serikali chenye mamlaka ya udhibiti utendaji na ushauri wa kuendeleza na kukuza biashara za ndani na nje ya nchi .

Alieleza kuwa dhima ya mamlaka hiyo ni kuwezesha ukuaji wa uchumi wa Tanzania kwa kuendeleza na kukuza bidhaa na huduma mbal mbali kwa masoko ya ndani na je ya nchi .

Kwa Upande wa Mkufunzi wa  Mafunzo hayo  Mshauri wa Mfumo wa Taarifa za Biashara TanTrade,Gema Mwikoko amesema iko haja ya Wakuu wa Taasisi kuwashajihisha wafanya biashara kujisajili  katika mfumo huo  ambao utawapatia  mbinu za kibiashara pamoja na kupata masoko ya kikandana na kimataifa.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.