Habari za Punde

Mhe Othman afanya ziara kuwatembelea wagonjwa


MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amefanya ziara maalum ya kuwatembelea na kuwajulia hali wagonjwa mbali mbali katika maeneo tofauti ya Mkoa wa mjini Magharib Unguja.

Akiwatembelea wagonjwa hao majumbani kwao, Mhe. Othman amewataka  wagonjwa wote  kuendelea na uvumilivu na subra kutokana na maradhi waliyonayo na kumuomba Mwenyezi mungu awape  shifaa ili wapone haraka na  waendelee na shughuli zao binafsi na kushiriki katika kazi ujenzi wa taifa.

Mhe. Othman, amewaeleza wagonjwa aliowatembelea kwamba maradhi ni mtihani kutoka kwa mola Muumba kuwakumbuka waja wake kwa namna tofauti na ni yeye pia mwenye uwezo wa kuponya maradhi yote.

Mhe. Othman katika ziara hiyo alimtembelea Kadhi Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji huko nyumbani kwake  Magogoni na Mwengine aliyemtembelea nyumbani kwake Magomeni kwa Ayuba ni Sheikh Khamis Yussuf ambaye ni Amiri wa Jumuiya ya Answari Sunna na pia ni Naibu Katibu wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA).

Aidha alimtembelea Katibu Mtendahi wa Jamuiya ya Maimamu Zanzibar huko nyumbani Kwake eneo la Saraevo katika wilaya ya Magharib B Unguna Sheikh Muhidin Zubeir na pia alimujulia hali ndugu Ali Abdalla Ali huko nyumbani kwake Chukwani Zanzibar.

Nao wagonjwa waliotembelewa wealimshukuru Mhe. Othman kwa uamuzi wa kuwajulia hali na  kusema kwamba wamefarajika sana na ujio wa mhe. Makamu  majumbani kwao ili kuwajulia hali na kumuomba aendelee na utaratibu huo kwa kuwa ni jambo jema na linaridhiwa mwenyezi mungu  Muumba.

Mhe. Othman  amekuwa  akiwajulia hali wagonjwa na watu mbali mbali wasiojiweze katika kila baada ya vipindi  ikiwa ni utaratibu wake aliojiwekea.

Ziara kama hiyo aliifanya katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita ambapo aliwatembelea wazee na wagonjwa mbali mbali katika wilaya za Mjini na Magharib Unguja.  

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 24.01.2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.