NA
MWASHAMBA JUMA, IKULU
RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amewataka
wahitimu wa vyuo vikuu nchini kujikita kwenye tafiti zitakazotoa ufumbuzi wa
matatizo yaliomo kwenye jamii.
Aidha,
alivitaka vyuo vikuu kuongeza progam kwa mujibu wa mahitaji ya wakati uliopo na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia
duniani ili kuleta kuleta mabadiliko nchini
Dkt.
Mwinyi alitoka kauli hizo kwenye Mahafali ya 22 ya Chuo Kikuu cha Abdulrahman
Al- Sumait, Chukwani Wilaya ya Magharibi B, Unguja.
Aliwataka
wahitimu wa chuo hicho kutumia tafiti zao kwa lengo la kutatua changamoto
zilizomo kwenye jamii badala kuziweka tafiti hizo kwenye makbtaba na
kuzifungia.
Alizishauri
Wizara na Idara za Serikali kushirikiana na vyuo vikuu kufanya tafiti zenye
kuchochea maendeleo kwenye nyanja zote za jamii na uchumii, tehama na
mawasiliano ili kutela mabadiliko yenye
tija.
“Nazishauri
Wizara na Idara za Serikali kushirikiana na wataalamu wa vyuo vikuu vyetu,
kufanya tafiti zitakazosaidia kuchochea maendeleo katika nyanja za kijamii,
uchumi na teknolojia ya habari na mawasiliano ili kuendelea kusonga mbele”
Alishauri Rais Mwinyi.
Katika
hatua nyengine Rais Dk. Mwinyi, aliwasihi wahitimu hao kwa watakao bahatika ajiriwa
ama kujiajiri wenyewe baada ya kuhitimu mafunzo yao, wakafanyekazi kwa uadilifu,
kujituma na kuchunga maadili mema yanayokubalika katika jamii ili waongeze tija
kwa kuleta mabadiliko kwenye utendaji wao.
Aidha, aliwataka
wakawe wabunifu wa kuzitafuta fursa za kujiendeleza zaidi na kuzitumia kwa
weledi na ufanisi wa hali ya juu kwa lengo la kujiimarisha kitaaluma.
Hata
hivyo, aliwaasa wanafunzi wanaoendelea na masomo chuoni hapo kuendelea
kudumisha nidhamu na kufuata mazuri ya watangulizi wao kwa kuwa na maadili mema
ya kutafuta elimu ili wapate ufaulu mzuri
Akizungumza
kwenye mahafali hayo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Lela Muhamed Mussa aliwataka
wahadhiri wa chuo hicho kujikita zaidi kwenye kutoa elimu ya ufundi na mafunzo
ya amali ili kuwapa uwezo wanafunzi wakujiajiri wanapokamilisha masomo yao.
Alisema Sera
ya elimu inawataka wanafunzi watakapomaliza masomo yao yalazima kwa ngazi ya
sekondari, kuwe na sehemu ya wao kupata kujiendeleza kwa ustadi na ufundi.
Alisema Serikali
inania ya kutanua wigo kwenye skuli za umma kwaajili ya wanafunzi kujikimu
pamoja na kuwana taasisi ama vyuo vitakavyo wawezesha wanafunzi kujiari baada
ya mafunzo yao.
“Lazima
tuwe na taasisi, tuwe na vyuo mbalimbali vyenye kutoa fani tofauti ambazo
wanafunzi wataweza kujiajiri baada ya
masomo yao” Alishauri Waziri Lela.
Alisema
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka kipaumbele zaidi kwenye mafunzo ya
Amali ili kuwapa uwezo wanafunzi wanaomaliza masomo yao wajirike.
Alisema kuanzishwa
kwa Chuo Kikuu cha Sumait kumekua msaada mkubwa katika kuendeleza juhudi za Serikali.
Kwa
upande wake Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Msafiri Mshewa aliwataka wahitimu
hao wakasaidie kuleta mabadiliko chanya
kwenye jamii zao kwa kuutumia vizuri ujuzi wa taaluma zao kuongeza tija, aidha,
aliwataka wakawe mabalozi na kuzikimbilia fursa kwa kuzifanyia kazi zenye tija.
“Ni
matumaini yetu elimu mliyoipata itawanufaisha nyinyi, jamii na Watanzania kwa
ujumla, kila mmoja wenu anawajibu na nafasi ya kuchangia maendeleo kwa kuangalia eneo la taaluma yake
litakavyosaidia kuleta mageuzi ya maendeleo kwa kuajiriwa ama kujiajiri wenyewe”
Aliwaasa wahitimu hao.
Chuo cha
Abdulrahman Al Sumait chini ya uongozi wa Mkuu wake, Dk. Aman Abeid Karume,
Rais Msaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar awamu ya sita, kina jumla ya
wanafunzi 4553 tokea kuanzishwa kwake mwaka 1998. Jumla ya wahitimu 310
wakiwemo wanawake 183 na wanaume 127 walikamilisha masomo yao na kuhuduria
kwenye mahfali ya 22 ya chuo hicho
Wahitimu
18 kati yao walitunukiwa shahada ya udhamili, 241 shahada ya kwanza na 51
walitunukiwa stashahada na astashahada.
No comments:
Post a Comment