Habari za Punde

Bonanza la Michezo Shehia ya Pangawe

Katibu  Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar  Salum Issa Ameir akikagua timu ya mpira wa miguu Dogo dogo FC wakati wa ufunguzi wa Bonanza la Michezo la Shehia ya Pangawe Wilaya ya Magharibi “B”lililofanyika huko Uwanja wa Mpira wa Nyarugusu
Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar Salum Issa Ameir akikabidhi fomu ya kujiunga na Baraza kwa mmoja wa wachezaji wa Timu ya mpira wa miguu Boda boda FC katika Bonanza la Michezo la Shehia ya Pangawe Wilaya ya Magharibi “B” lililofanyika huko Uwanja wa Mpira wa Nyarugusu.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar akikabidhi soda kwa mmoja wa wachezaji wa timu ya Nage katika Bonanza la Michezo la Shehia ya Pangawe  Wilaya ya Magharibi “B” lililofanyika huko Uwanja wa Mpira wa Nyarugusu

Bahati Habibu                         BVZ Zanzibar

 Katibu Mtendaji Baraza la Vijana Zanzibar Salum Ameir Issa amewata vijana Nchini kuitumia michezo kuwa fursa ya kujiajiri na njia itakayowafanya kujikinga na vitendo vya udhalilishaji pamoja na kujiepusha na matumizi mabaya  ya dawa za kulevya.

Kauli hiyo ameitowa huko shehia ya Pangawe Wilaya ya Magharibi “B” mkoa wa Mjini Magharibi  wakati akifungua Bonanza la Michezo la kuwahamasisha  Vijana wa Shehia hiyo kujiunga na Baraza hilo.

Amesema kumekuwa na wimbi kubwa  la kesi zinazo wakabili vijana kwa makossa yatokanayo na vitendo vya udhalilishaji na matumizi ya dawa za kulevya jambo ambalo ni hatari hasa ikizingatiwa vijana ndio  tegemeo la dadae  kwa ujenzi wa Taifa.

Amesema hali hiyo ilisababishwa na vijana kujiachia na kuzurura bure na hatimae kutumbukia katika hali mbaya ya vitendo vibovu.

Amesema vijana wajiunge na baraza hilo ili liweze kuwasaidia na kuweza kuwatatulia changamoto zinazo wakabili.

“Nakuombebi vijana mjiunge na baraza hili ili kupata fursa zinazotolewa na  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia taasisi hiyo”alisema katibu Salum Ameir.

Aidha amefahamisha kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Baraza la Vijana inaendelea kuwapatia vijana elimu ya ujasiriamali kwa kuwapeleka Vijana katika Vyuo vya Mafuzo vya amali sambamba na kuwapatia mitaji itakayo wafanya wajiajiri baada ya kuhitimu mafunzo hayo.

“Niwaambie Vijana wenzangu ni muhimu kujiunga na Baraza hii itatusaidia kuwa na uzalendo wa  kulinda nchi yetu na kutambua fursa za kiuchumi zilizomo nchini.” Alisema Katibu huyo.

Nae Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Shehia ya Pangawe Iddi Ali Ame amesema michezo imekuwa ni sehemu ya ajira hivyo amewataka vijana kushiriki michezo kwa lengo la kuimarisha afya na kuonyesha vipaji vyao vitakavyowasaidia kujiajiri au kuajiriwa.

Katika bonaza hilo Michezo mbali mbali imechezwa  ikiwa ni pamoja na mpira wa miguu na mpira wa nage sambamba na utolewaji wa fomu za kujiunga na Baraza la Vijana Zanzibar kwa washiriki wa Bonanza hilo.


 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.