Ndege jamii ya Pentiole ambaye utafiti umebani amehamia katika nkatika hifadhi ya Taifa ya Mazingira asilia Mwambesi wilayani Tunduru mkoani Ruvuma kutoka nchini Madagasca
MSITU wa Hifadhi wa
Taifa wa mazingira asilia Mwambesi uliopo wilayani Tunduru mkoani Ruvuma
ulianzishwa mwaka 1956 na ulipandishwa hadhi kuwa msitu wa Taifa katika kipindi
cha mwaka 2017/2018.
Meneja wa Huduma za
Misitu Tanzania (TFS) wilayani Tunduru Denis Mwangama anasema msitu huo
umepandishwa hadhi ili kuongeza uhifadhi zaidi kutokana na kuwa na utajiri wa
viumbe vya kipekee duniani wakiwemo wanyama,ndege na mimea.
Anawataja wanyama waliopo
katika msitu huo ambao upo kando kando mwa Mto Ruvuma kuwa ni simba, tembo, chuo,kuro,jamii
za nyani,jamii za swala,nyati na wanyama wengine.
Mwangama anasema
Katika msitu wa Mwambesi kuna jamii ya ndege maarufu duniani anayeitwa Pentiole
ambaye utafiti uliofanywa na PALMS Foundation mwaka 2015 umebaini kuwa ndege
huyo amehamia kutoka nchi ya Madagaska baada ya mazingira aliyokuwa anaishi
kuharibiwa na shughuli za kibinadamu.
Kwa mujibu wa
Mwangama, ndege huyo ana tabia ya kuzamia samaki kutoka majini na kwamba ndege
hao wanapenda kuishi kwenye maporomoko ya
Mto Ruvuma yanayoitwa sunda ambayo yapo ndani ya hifadhi hiyo.
“Tanzania tuna bahati katika msitu wetu tuna ndege Pentiole ambaye amekuwa akiishi ukingoni mwa maporomoko ya
maji yajulikanayo kama Sunda Water falls’’,anasisitiza.
Kwa mujibu wa Mwangama Ndege huyu huogolea kwankufuata mdondoko wa mawimbi ya maji kwenye maporomoko hayo akitatafuta mawindo
yake ya samaki ambacho ndicho chakula chake pekee.
Licha ya ndege huyo
Mwangama anayataja maporomoko ya Sunda kuwa ni miongoni mwa vivutio vya utalii
katika hifadhi ya Mwambesi na kwamba maporomoko hayo yalitumika wakati wa vita
ya Majimaji kati ya mwaka 1905 hadi 1907
ili kujificha kwenye mapango kwa juu.
Anasema Mto huo ndio uliokuwa ukitumika kwenye vita vya Majimaji ambapo
watu wa makabila au ukanda wa kusini
hususani Wangoni walitumia maji yake
katika kuzimia silaha za moto chini ya uongozi wa Kinjeketile Ngwale.
Kulingana na Mwangama, eneo hilo pia linaaminika Wajerumani walitumia
kama njia kubwa wakitokea Msumbiji katika biashara ya meno ya Tembo na kwamba Waarabu
walipita pembezoni mwa mto huo kuwapitishia watumwa.
Hata hivyo anasema
awali kabla ya serikali kuamua msitu huo kuwa Msitu wa hifadhi,kulikuwa na
vitalu vya uwindaji wa kitalii ambapo ndani ya msitu kulikuwa na kambi ya wawindaji
iliyoitwa Big Game iliyoendeshwa na Kampuni ya
uwindaji iliyoitwa Tandara Hunting Safaris.
Kulingana na Meneja
huyo,msitu huo una ukubwa wa zaidi ya hekta 112,000 na kwamba mtalii akiwa katika
msitu wa Mwambesi anaweza kufanya utalii wa kuteleza kwenye mitumbwi katika mto
Ruvuma.
Deborah Mwakanosya ni
Meneja wa Msitu anasema Mwambesi ni
msitu wa asili wa pili kwa ukubwa kwa Tanzania ukiongozwa na msitu wa Kilombero
mkoani Morogoro.
Anasema msitu huo
ambao umezungukwa na mto Ruvuma, umesheheni baianowai mbalimbali za mimea adimu
duniani ikiwemo miti aina ya mipozipozi ambayo ina tabia ya kudondosha maji
inapatikana sehemu chache duniani ukiwemo msitu wa Mwambesi.
Mwambesi ni moja kati ya Misitu mikubwa ya Hifadhi za Mazingira Asilia
tulionayo wenye utajiri mwingi wa flora na fauna zakutosha.
Msitu wa Mwambesi unahifadhiwa kisheria chini ya
uangalizi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwa kushirikina na Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) Kanda ya Kusini.
Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
No comments:
Post a Comment