Alisema taasisi hizo ndizo
zinazowalea vijana kiimani, weledi, ujasiri na uzalendo kwa taifa na viongozi
wao jambo ambalo linaimarisha amani na uthubutu wa kufikia maendeleo.
Rais Dk. Mwinyi
aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na uongozi wa Jumuiya ya Sunni
Jamaat waliofika kujitambulisha.
Alisema taasisi binafsi na za
kidini zinajukumu la kuisaidia Serikali kuendeleza huduma za jamii pia
aliishukuru jumuiya hiyo kwa juhudi za kuendeleza elimu Zanzibar.
Aidha, alizitaka jumuiya za dini kuendelea
kuishauri Serikali kwa mawazo yatakayojenga na kuleta ufanisi kwenye misingi ya
maendeleo ya taifa, hata hivyo aliishukuru taasisi hiyo kwa mchango wanaoutoa
kwenye sekta ya elimu.
Dk. Mwinyi alizungumzia
changamoto zinazoikabili sekta ya elimu zikiwemo uhaba wa vifaa vya maabara,
maktaba, kuongeza madawati, kompyuta na vitabu, pia kuondoa mikondo kwa
wanafunzi. Hata hivyo, alisema Serikali ya awamu ya nane imejenga skuli 48 kati
ya hizo 10 za ghorofa.
“Kwa hatua tuliyofikia matokeo
yanaweza yasionekane leo, maana ukianza kuigeuza elimu faida yake itaonekana miaka
mingi baadae.” Alifaafnua Rais Mwinyi.
Alisema Serikali pia inafanya
utafiti wa kina kutafuta suluhu ya wanafunzi wengi kufeli na kuweka mikakati
imara itakayoinua sekta ya elimu, Zanzibar.
“Safari hii tumeamua kufanya
utafiti maana changamoto za elimu ni nyingi mno kila kona huwezi kuziepuka,
kuanzia idadi ya wanafunzi kwenye madarasa ndio maana tunajenga skuli mpya ili
kupunguza idadi ya wanafunzi wengi madarasani” alifahamisha Dk. Mwinyi.
Alisema serikali pia inaangalia
upya mfumo wa elimu ambao wanafunzi wengi huanza msingi lakini wanaoingia
vyuoni ni wachanche hivyo inaangalia kundi la katikati linalofeli ambalo ni
kubwa.
Wana Jumuiya hao walimshukuru Dk. Mwinyi kwa juhudi ya kuipambania
sekta ya elimu nchini na kueleza kuwa wameshuhudia mafanikio makubwa ndani ya
miaka miwili ya uongozi wake hasa kwenye
kutoa kipaumbele kuimarisha huduma za jamii .
Walitumia fursa hiyo kuusifu
kwa uongozi wake mahiri ambao waliueleza kwamba unaendelea kudumisha amani
niliopo.
IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment