RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi amewasihi wadhamini na wadau wote walioungamkono maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislam kutochoka kuendeleza juhudi zao kila mwaka wa maadhimisho hayo.
Al
hajj Dk. Mwinyi aliyasema
hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na kamati ya maandalizi ya maadhimisho ya
mwaka mpya wa Kiislam 1445 H yaliyoadhimishwa mwaka huu, kisiwani, Pemba kwa
nia ya kuwashukuru.
Aliishukuru Kamati, viongozi
wote wa dini pamoja na wadhamini waliochangia na kushiriki bega kwa bega hadi
kufanikisha maadhisho hayo ya mwaka mpya wa kiislam 1445 H.
“Nichukue fursa hii
kuwashukuru wadhamini wote wengine mpo hapa na hata waliokuwa hawapo, mkisikia
tu tuna kushukuruni mjue tunakuhitajini tena, kwa hiyo msochoke sababu
maadhimisho haya yatakua kila mwaka katika kuadhimisha mambo ya heri” alisihi,
Al hajj Dk. Mwinyi.
Al hajj Dk. Mwinyi
alieleza Serikali ilipokea kwa uzito mkubwa ombi la Kamati hiyo la siku ya
mapumziko ya kitaifa kila ifikapo maadhimisho ya mwaka huo na kueleza shukarani
zake kwa kamati hiyo kwa kuja na hoja hiyo ambayo ilikuwa na mafanikio makubwa
na kueleza tukio la ugawaji vyeti vya shukrani kwa kamati hiyo ni ishara ya
kukubalika kwa hatua ya mafanikio waliyoikamilisha.
Akizungumza kwenye
hafla hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mwl. Haroun Ali Suleiman, alishukuru ushirikiano uliopo baina ya
Serikali na kamati hiyo hadi kufanikishwa kwa maadhimisho ya mwaka mpya wa
Kiislam 1445 H ambao alieleza kupokelewa vizuri kwenye jamii.
Naye, Mfti Mkuu wa
Zanzibar, Sheikh Saleh Omar Kaabi alimshukuru Al hajj Dk. Mwinyi kwa mwitikio
wake na ushirikiano anautoa kwa Ofisi ya Mufti na kushiriki vyema kwenye mambo
yenye heri.
Alisema, kuanzishwa
kwa jambo hilo kitaifa ni neema kubwa ya kuendeleza mambo mema kwa jamii na
taifa kwa ujumla.
Akiwasilisha taarifa
ya shukurani kwa Serikali kutokana na maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislam 1445
H, Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti, Sheikh Khalid Mfaume, alisema lengo la
maadhimisho yam waka huo ni kuitangaza tarehe ya kiislam na kuendeleza historia
ya dini walioiacha maulamaa na kuahidi ofisi ya Mufti inajukimu ya kuendelea
kuitangaza tarehe hiyo kwa kuishajisha kwa jamii kuendelea kutenda mema.
Aliishuru Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuthamini maoni ya wananchi wake baada ya kupokea
ombi ya siku ya mapumziko kila ifikapo siku maadhimisho ya mwaka mpya wa
kiislam kila mwaka.
Maadhimisho ya mwaka
mpya wa Kiislam 1445 Hijria, yaliadhimishwa masjid Munawwara, uliopo eneo la Mfikiwa
Mkoa wa Kusini, Pemba ambako Mgeni rasmi alikua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi, Al Hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi na kuhudhuriwa na
viongizi wengine wa dini na kitaifa kwa kutanguliwa na matukio mbalimbali
ikiwemo kutoa huduma za matibabu ya macho kwenye hospitali ya kivunge, Mkoa wa
Kaskazini Unguja, kusomwa dua ya kuliombea Taifa, kufanikishwa kwa kongamano
kuwa la wanawake wa Kiislam lililohudhuriwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,
Hajjat Dk. Samia Suluhu Hassan kwenye ukimbi wa Golden Tulip Uwanja wa ndege, Zanzibar,
maonesho ya kiislam ya biashara yaliyowashirikisha wafanyabiasha wadogo na
wajasiriamali, matembezi ya Zafa, kisiwani Pemba yaliolenga kuboresha
afya pamoja na matembezi ya hiari yalifanyika Unguja.
IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment