Habari za Punde

Mhe Othman azungumza na viongozi mikoa, ngome za wanawake na wazee, pamoja na Viongozi wapya wa Matawi ya chama cha ACT Wazalendo

MAKAMU Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Msoud Othman, akizungumza na viongozi wa  Mikoa , Ngome ya wazee , vijana na wanawake wa chama hicho pamoja na viongozi wampya wa  ,matawi waliochaguliwa hivi karibuni. Mkutano huo umefanyika huko katika Ukumbi wa Majid Kiembesamaki wilaya ya Magharib ‘B’ Unguja leo tarehe 03.09.2023.  Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
MAKAMU Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Msoud Othman, akizungunza na viongozi wa  Mikoa , Ngome ya wazee , vijana na wanawake wa chama hicho pamoja na viongozi wampya wa  ,matawi waliochaguliwa hivi karibuni. Mkutano huo umefanyika huko katika Ukumbi wa Majid Kiembesamaki wilaya ya Magharib ‘B’ Unguja leo tarehe 03.09.2023.  Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Baadhi ya Viongozi  wa  Mikoa , Ngome ya wazee , vijana na wanawake pamoja na viongozi wampya wa  matawi waliochaguliwa hivi karibuni wa ACT Wazalendo wakimsikiliza  Makamu Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Msoud Othman, alipowahutubia katika mkutano wa viongozi hao uliofanyika huko katika Ukumbi wa Majid Kiembesamaki wilaya ya Magharib ‘B’ Unguja leo tarehe 03.09.2023.  Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.



Baadhi ya Viongozi  wa  Mikoa , Ngome ya wazee , vijana na wanawake pamoja na viongozi wampya wa  matawi waliochaguliwa hivi karibuni wa ACT Wazalendo wakimsikiliza  Makamu Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Msoud Othman, alipowahutubia katika mkutano wa viongozi hao uliofanyika huko katika Ukumbi wa Majid Kiembesamaki wilaya ya Magharib ‘B’ Unguja leo tarehe 03.09.2023.  Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.


MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha ACT- Wazalendo Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewataka  Viongozi wa Matawi  wa Chama hicho waliochaguliwa kwenye uchaguzi wa ndani wa hivi  kuelewa kwamba wao ndio msingi muhimu unaobeba  dhima ya kuwapata viongozi bora katika ngazi za majimbo, wilaya na mikoa wenye uwezo wa kusaidia kujenga chama na kupata ufanisi  mkubwa ili kutimiza  malengo ya chama hicho yaliyowekwa.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko ukumbi wa Majid Kiembesamaki  Wilaya ya Magharib Unguja, alipozungumza na viongozi  mikoa, ngome za wanawake na wazee, pamoja na Viongozi wapya wa Matawi ya chama hicho kutoka Mikoa yote ya Unguja Kichama, kufuatia  kukamilika uchaguzi wa Viongozi wa matawi hivi karibuni.

Mhe. Othman ambaye pia ni makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar , amefahamisha kwamba kuwepo kwa viongozi hao makini pia ndio msingi madhubuti katika kujenga na kuimarisha chama hicho ambao watasaidia   kuendeleza jitihada za kufanikisha maelngo na dhamira ya chama hicho ya kuwepo Zanzibar yenye umoja na mshikamano wa kuiletea maendeleo Zanzibar.

Amefahamnisha kwamba chama hicho kinahitaji viongozi makini watakosaidia jitihada za chama hicho ya kuwepo Zanzibar moja na kuwataka kwenda kufanyakazi za kutumikia chama kwa juhudi kuwa katika kutimiza maono ya chama hicho kwa kuzingatia uzalendo wa kuipoenda nchi yao.

Aidha amewataka  viongozi hao  waliochaguliwa kujenga  mashirikio makubwa na  uongozi wa ngome zote za chama hicho ili kuweza kujenga taasisi imara itakayowezesha kukipatia ushindi chama hichi katika uchaguzi mkuu  ujao wa mwaka 2025.

Mhe. Othman amesema kwamba kufanyika kwa chaguzi hizo katika misimingi ya kidemokrasia ni kelelezo muhimu kinaochonesha kwamba hakuna walikwenda kupanga safu kwa kuwabeba baadhi ya wagombea lakini  ni wale waliofahamu wajibu na dhamira ya chama hicho ya kuijenga Zanzibar mpya.

Makamu mwenyekiti huyo amewapongeza viongozi walichanguliwa na kuwataka kutokulala na badala yake wafanye kazi kubwa ya kukitumikia chama sambamba na kuwashukuru wagombea walioshindwa kwa kuonesha ukomavu na kwamba kushindwa kwao hakuoneshi kwamba ni dhaifu kwa kuwa chama hicho kinahazi kubwa ya viongozi  wengi wazuri katika kusimamia safu mbali mbali.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zanzibar ambaye pia ni waziri wa Afya Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui amewataka vijana wa chama hicho kutorudi juma na badala yake waendeleze umoja na msihakamano jutakaosaidia kupatikana mafanikio ya chama na Zanzibar kwa jumla.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Ismail Jussa Ladhu amewataka vijana kuelewa kwamba wao ni tegemeo kubwa la maendeleo na umoja wa Zanzibar na kwamba kuna haja ya kujifunza na kuelewa masuala mbali mbali yanayohusu historia ya Zanzibar katika kusaidia ujenzi wan chi yao.

Mapema Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chama hicho Said Rashid Muhene amesema kwamba kazi ya uchaguzi wa viongozi ngazi yay a matawi ya chama hicho unguja na Pemba imefanyika kwa ufanisi  mkubwa na kwanga hivi karibuni utaendelea katika kuwapata vuiongozi wapya wa ngazi ya majimbo.

 


Kitengo cha Habari ,

Ofisi ya Makamu wa Kwanzawa wa Rais Zanzibar

Septemba 03, 2023.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.