Habari za Punde

RC kusini asisitiza mashirikiano dhidi ya vita vya udhalilishaji

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid Rashid akizungumza na wazazi,walezi na wanafunzi  kuhusu uwepo wa  Vitendo vya Udhalilishaji huko Skuli ya Bambi Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Mkuu wa Wilaya ya Kati Marina Thomas akizungumza na wazazi,walezi na wanafunzi  kuhusu uwepo wa  Vitendo vya Udhalilishaji huko Skuli ya Bambi Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Wazazi,Walezi na Wanafunzi wakisikiliza kwa makini nasaha kuhusu vitendo vya udhalilishaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid Rashid (hayupo pichani) huko Skuli ya Bambi Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

PICHA NA FAUZIA MUSSA –MAELEZO ZANZIBAR


Na Fauzia Mussa,      Maelezo 


 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid Rashid amewataka Walezi kushirikiana  na Walimu  ili kuondokana na vitendo vya udhalilishaji.

 

Akizungumza na wazazi,walezi,walimu na wanafunzi huko Skuli ya Bambi Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja amesema  vitendo hivyo vimekua vikigharimu na kukatisha malengo ya watoto hao siku hadi siku.

 

Alisema jukumu la kupinga vitendo vya udhalilishaji si la Serikali pekee   bali jitahada za pamoja zinahitajika ili kutokomeza vitendo hivyo.

 

“kila mmoja ni mchunga na ataulizwa juuu ya alicokichunga” alinukuu Mkuu huyo

 

Aidha  aliwataka Walezi kusimamia vyema maelezi ya watoto wao ili kuwakinga na vitendo hivyo kwani endapo watawaachia walimu  pekee tatizo hilo litakua endelevu.

 

Alifahamisha kuwa endapao jamii itaacha vitendo vya udhalilishasji vitawale kuna hatari ya kukosa viongozi shupavu  wa baadae.

 

“ tukiicha hali hii iendelee hatutakua na mashehe,viongozi wala walimu katika nchi yetu”alifahamisha Mkuu huyo.

 

Nae  Mkuu wa Wilaya ya Kati Marina Thomas amewataka wazazi kukaa karibu na watoto wao na kufatilia nyendo zao kwa  kuwadadisi ili kuweza kugundua uwepo wa vitendo hivyo katika hatua za awali.

 

Kwa upande wake Mwalimu mkuu Skuli ya Msingi Bambi Muhammed Ramadhan Mapuri amewaomba Walezi kuwachunga watoto wao kutokana na vikundi vya madawa ya kulevya kwani kunachangia uwepo wa vitendo vya  ubakaji,udhalilishaji  na unyanyasaji wa kijinsia.

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.