Habari za Punde

Ukarabati wa Hospitali ya Abdalla Mzee wakamilika



 WIZARA ya Afya Zanzibar imetiliana saini mkataba na Serikali ya China ya kukabidhiwa mradi wa Hospitali ya Abdalla Mzee ya Mkoani Pemba baada ya kufanyiwa ukarabati Mkubwa na utanuzi wa Hopitali hiyo na Serikali ya China.

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui amesema mradi huo ambao umeanza mwaka 2020 umehusisha kuongeza Majengo na kufanya matengenezo makubwa na kuongeza idadi ya vitanda kufikia 160 kutoka vitanda 80 vilivyokuwepo awali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.