Habari za Punde

Wajasiriamali Wakabidhiwa Nishati Safi ya Kupikia Zanzibar

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, kazi, Uchumi na uwekezaji Mhe.Shariff Ali Shariff akimkabidhi jiko la gesi Mwenyekiti wa UWT  Mkoa wa Mjini Magharibi Ghanima Sheha Mbwara , ikiwa ni Mpango maalumwa Serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wote na kutunza mazingira, hafla iliyofanyika Rahaleo Zanzibar.

Na Sheha She.Maelezo. 10.04.2024.

Zaidi ya Wanawake Wajasiriamali 100 wa Mkoa wa Mjini magharibi wamekabidhiwa Majiko ya Gesi ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa wote.

Akizungumza katika Shughuli ya kukabidhi majiko kwa Wajasiriamali hao huko Rahaleo, Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, kazi, Uchumi na Uwekezaji Mhe. Sharif Ali Sharif amesema majiko hayo yatawawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Waziri Sharif amesema Nishati ya gesi ni muhimu kwa ajili ya kulinda afya za watumiaji pamoja na utunzaji wa Mazingira kutokana na kupunguza matumizi ya rasilimali ya Misitu.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum amewataka Wajasiriamali kulipa kodi kihalali ili kuwewezesha Serikali kupata mapato na kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Naye Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita ameishukuru Kampuni ya ORYX ENERGIES kwa mchango wao wa Majiko hayo ambayo yatawarahisishia Wajasiriamali hao katika Shughuli zao na kuwakinga na madhara yatokanayo na matumizi ya kuni ikiwemo moshi.

Naye Meneja Mkuu wa ORYX ENERGIES Kanda ya Zanzibar, Ndg. Shuweikha Khamis Juma amesema Kampuni hiyo imetoa msada huo ili kuwasaidia wanawake hao kuondokana na athari zianazoweza kutokana na matumizi ya nishati ya kuni ikiwemo magonjwa mbalimbali.

Nao Wanawake Wajasiriamali walionufaika na Majiko hayo Wameushukuru Uongozi wa ORYX ENERGIES kwa kuwapatia majiko hayo na kuahidi kuyatumia Vyema ili lengo lililokusudiwa liweze kutimia.







No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.