MKOA
WA KUSINI UNGUJA,
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Mhe. Othman Masoud Othman, amezitaka mamlaka zinazosimamia raslimali ya
ardhi kuchukua hatua sahihi na pia kuwasaidia
wananchi kushirikiana kurejesha hali ya maeneo yaliyoharibika kwa kuchimbwa
mchanga ili ardhi hiyo iweze kuzalisha kwa tija na kuwa na manufaa zaidi.
Mhe. Othman ameyasema hayo
alipotembelea eneo la Pangatupu Wilaya ya Kaskazini B Unguja lilioharibika
vibaya kwa kuchimbwa mchanga ambalo lipo katika Mpango wa Taifa wa Kuirithisha
Zanzibar kuwa ya kijani unaotarajiwa kuwa shirikishi kwa taasisi na makundi
yote ndani ya jamii .
Amesema kwamba pamoja na mahitaji ya matumizi
ya mchanga yaliyipo ambayo kimsingi hayawezi kusita, lakini kuna haja kubwa ya kuwepo usimamizi bora
wa maeneo hayo kwa kuwa na matumizi sahihi bila kuendelea kuharibika kwa maeneo
yaliyoruhusiwa kuchimbwa mchanga.
Amefahamisha kwamba ni muhimu kuwepo
na utaratibu wa kuyatumia maeneo yaliyoriuhusiwa kisheria na kabla ya kuhamia
kwenye maeneo mengine kuhakikisha yanarekebishwa na kurejeshwa katika hali yauasili
ili pia yaendelea kutumika kwa
uzalishaji wa kilimo na mazao mengine ikiwemo upandani wa minazi, miti ya
matunda na aina nyenginezo.
Amesema hali ilivyo sasa inaonesha
athari ni kubwa sana jambo ambalo ni funzo kubwa kwa nchi katika kuhakikisha
kwamba pale eneo linapotumika kuchimbwa mchanga kunakuwepo na utaratibu bora ambao
hautaharibu mazingira ya eneo husika kama ilivyo sasa ili kuepuka athari kubwa kwenye ardhi mbali mbali za
Zanzibar zilizochimbwa mchanga.
Amesema kwamba iwapo kutakuwa na
utaratibu wa aina hiyo na kuwa endelevu kutaisaidia sana Zanzibar kuendelea
kuwa ya kijani jambo ambalo hivi sasa linaonekana kupotea na ndio maana
serikali imekuwa na mpango huo wa kuirithisha Zanzibar kuwa ya kijani.
Amefahamisha kwamba ni busara
kutengeneza mpango sahihi wa kuyafufua maneo yote yaliyoharibika kwa kuwasaidia
wananchi pamoja na kuwaelimisha kuilinda ardhi ndogo iliyopo na kuitumia neema hiyo kwa tija
kubwa katika uzalishaji wa mazao mbali mbali ikiwemo upandaji wa minazi
inayoweza kuzalisha vyema kuliko ilivyo sasa.
Wakati huo huo, Mhe. Makamu amewataka
wataalamu wa Kilimo wanaosimamia uzalishaji wa miche ya miti ya chakula na
matunda Zanzibar kuhakikisha kwamba
wanatumia utaalamu wa kileo ikiwemo tekenolojia ya kisasa ili kuwawezesha
vijana kuvutika na kuwa na mwamko mkubwa zaidi wa uzalishaji wa mazao kupitia
teknlojia hiyo.
Amefahamisha kwamba nchi mbali mbali duniani
zilizopata mafanikio katika maendeleo ya kilimo zimejitahidi kuitumia vyema kwa
pamoja sayansi na teknolojia pamoja na
maarifa ya Sanaa za kisasa katika uzalishaji wakileo unaoleta mafanikio ya
haraka.
Amesema hali hiyo inawezakana pia
kutumika Zanzibar lakini muonekano wa kituo cha uatikaji mbegu na uzalishaji wa
miche kilichopo Mwanyanya wilaya ya Magharib A Unguja haiakisi mahitaji ya
kisasa na kuwapa matumaini wananchi kwa kujengea ushawishi vijana wa
Zanzibar kupenda kushiriki katika kazi
za kilimo cha aina mbali mbali.
Amesema kwamba kunahaja na
inawezekana kutumia utaratibu wa tetknolojia ya kisasa kufanya mageuzi makubwa
kwenye sekata ya kilimo cha kuotesha miti ya matunda kuwa na miti midogo
inayoweza kuzalisha matunda mengi na kuleta tija kubwa kiuchumi kwa wananchi.
Mhe. Othman katika ziara hiyo
ametembelea eneo lilochimbwa mchanga la Pangatupu Kaskazini B, eneo
linaloteshwa miche ya mikoko Mtowapwani
Fungurefu Kaskazini A, eneo lililopandwa miti la Chaani Masingini pamoja na
Nasari ya uatikaji wa miche ya miti ya matunda na mazao mbali mbali ya Kilimo
huko Mwanyanya wilaya ya Magharib A.
No comments:
Post a Comment