Habari za Punde

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kupitia Chama Cha NRA Amechukua Fomu Tume ya Uchaguzi INEC

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA), Mhe. Hassan Kisabya Almas. Mgombea huyo wa NRA aliyeambatana na Mgombea Mwenza, Mhe.  Hamisi Ally Hassan (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 9,2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. Kualia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhan Kailima. (Picha na INEC).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.