6/recent/ticker-posts

SMZ Yakiri Malalamiko Wauzaji wa Karafuu Pemba.

Na Mwandishi Wetu.
Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko imekiri kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa Wakulima wa zao la Karafuu, Wananchi na wauzaji wa karafuu hasa kisiwanin Pemba kwamba wanapouza na kupimiwa karafuu zao kituo cha ZSTC zinapofikia bakaaya nusu au robo huwa hawalipwi na badala yake hulipwa kilo nzima.

Naibu Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Mhe. Thuwaiba Kisasi,aliyasema hayo katika baraza la Wawakilishi wakati ajibu suala la mwakilishi wa Jaku Hashim Ayoub,(Muyuni) aliuliza kwa nini Serekali haitowe kauli juu ya malalamiko hayo ya Wakulima wa Zao la Karafuu na Wauzaji wa karafuu kupata hakin yaohata kama ni kiwango  kidogo.

Waziri Kisasi alisema baada ya Wizara hiyo kufuatiliamalalamiko hayo imegunduwa kuwa malalamiko hayo hayana ukweli kwa sababu mezani zinazotumiwa na Shirika la ZSTC kwa kupimia karafuu wakati wanapozinunua zina vipimo vyote kuaznzia kilo moja hadi robo kilo na zinatumika ipasavyo.

Katika kuhakikisha mauzo hayo yana kumbukumbu za ununuzi wa karafuu za kila siku na za kila mkulima anaekwenda kuuza karafuu katika kiwango chochote kile huwa zinaingizwa katika daftari la manunuzi katika kituo hicho. Aliliambia baraza hilo.


Hata hivyo, alisema kwa bakaa ya karafuu ambazo ni kidogo kiasi kwamba hadhikidhi kiwango cha robo kilo Shirika la SZTC humrejeshea mkulia mwenyewe karafuu hizo na sambamba na hayo alisema kuwa shirika la SZTC .Litaendelea na kuchukuwa jitihada za kuwaelimisha zaidi wakulima wa karafuu ili waelewe vipimo sahihi vinavyotumika katika kupima mazao au karafuuzao.      

Post a Comment

0 Comments