6/recent/ticker-posts

Zaidi ya 400m/= Zatengwa Kukabiliana na Mabadiliko Tabia Nchi Zanzibar.

 Na Mwandishi Wetu.
Jumla ya shilingi milioni 400,000,000 zimetengwa kwa ajili ya programu maalum ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya Tabia Nchi kwa mwaka wa Fedha 2014/2015.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe. Fatma Ferej Abdulhabib, amesema kuwepo kwa mabadiliko ya tabianchi kuwa kubwa kumesababisha kutengwa kwa fedha hizo ili kukabiliana na hali hiyo.

Aidha alisema katika kipindi cha miaka miwili iliopita jumla ya shilingi1,316,752,700.0, zimeshatumika  kwa shughuli mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko tabianchi kupitia taasisi sita zinazohusika katika kutekeleza mradi huo.

Alisema fedha hizo zitapatikana kupitia programu ya kuendeleza Utalii Zanzibar na zitalenga zaidi katika kuendeleza ustawi na matumbawe ambayo yamekuwa yakiathiriwa na kupanda kwa joto la bahari na hatimae kufa hali ambayo imekuwa ikileta usumbufu kwa wavuvi pamoja na kupunguza haiba kwa watalii.

Waziri Fatma alieleza hayo katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi wakati akijibu suala la Mwakilishi wa jimbo la Wawi, Mhe. Saleh Nossor Juma, alitaka  kujua ni kiasi gani Serekali imepanua Bajeti ya Idara ya Mazingira katika suala zima la la kupambana na mabadiliko ya tabianchi Zanzibar.

’’Serekali inaelewa kuwa kiasi hicho cha fedha ni kidogo mno kukidhi mahitaji lakini hata hivyo imeamua kuaza kwa uwezo wake mdogo na kuendelea kufanya hivyo kadri hali itakavyoruhusu, ili kuhakikisha Zanzibar  inakuwa na uhakika wa upatikanaji wa fedha za mabadiliko ya tabianchi’’ alisema Waziri huyo.

Alisema katika kupambana na suala hilo pia Serekali imeanda mradi na kuhamasisha rasilimali za kuweza kutekeleza mradi huo.


Alifahamisha kwa kutambua suali la mabadiliko tabianchi ni kubwa linalohitaji fedha nyingi kulishughulikia Serekali ya Mapinduzi Zanzibar imeona ipo haja ya kuanzisha mradi huo ambao mwaka 2012 ilitiliana saini na Shirika la UNDP kupitia programu ya UNDP,kwa ajili ya kuuendesha mradi huo.

Hata hivyo alisema lengo kuu la mradi huo ni kujenga uwezo wa kuhimili na kusimamia mabadiliko tabianchini tatizo kubwa linaloikabili dunia hivi sasa ambapo nchi za visiwa kama Zanzibar ni maeneo ambayo yako hatarini zaidi kuathiriwa na athari hizo.

Pia alisema sekta mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kimazingira zimekuwa zikiathirika kwa kiasi kikubwa, kwani mabadiliko ya tabianchi yamekuwa ni tishio kwa maendeleo endelevu ya dunia na kikwazi kikubwa cha kufikia malengo ya melenia yaliyowekwa.

Waziri alibainisha chanzi kikuu cha kutokea kwa athari hizo ni kuongezeka kwa gesi ya ukaa kwenye usawa wa dunia.
Hata hivyo alisema Serekali imekuwa ikiendeleza jitihada mbalimbali za kuhakikisha kuwa mitaala ya skuli za msingi hadi vyuo vikuu inahusisha masuala ya mazingira ambapo kwa kuanzia Serekali imeingiza somo la mazingira katika ngazi ya msingi hadi Sekondari. 

      

Post a Comment

0 Comments