6/recent/ticker-posts

SMZ Yakiri Upungufu wa Wataalamu wa Kilimo.

Na Mwandishi Wetu.
Serekali ya Mapinduzi Zanzibar imeeleza kuwa bado wakulimawa zao la mpungawanaendelea kutumia mbegu yampunga ya Nerika licha ya wakilimahao kutoa kasoro kwa mbegu hizo na baadhi yao kutokuzitumia mbegu hizo katika kuzalisha zao la Mpunga Zanzibar.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo na Maliasili Zanzibar, Mhe Mtumwa Kheir Mbarak, katikakikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea nje kidogo ya mji wa Zanzibar huko Chukwani.

Kweli wapobaadhi ya wakulima hivi sasa wameacha kutumia mbegu ya Nerika na kutowa sababu kuwa mbegu hizo ni ngumu wakati wa kupiga, jambo linalowafanya baadhi yao kuacha kutumia mbegu hizo, lakini wapo baadhi yao wanaendelea kutumia mbegu hizo. Alisema.

Alisema licha  ya kuwa na kasoro hiyo ambayo wakulima wameitoa lakini wengi wao wameipokea vyema na wanaipenda sana.


Hata hivyo Naibu Waziri huyoamesema kuwa hawawezi kuwalazimisha wakulima kutumia mbegu hiyo

Kwa upande wa ukosefu wa mabwawa na mabibi shamba, alisema kuwa hivi sasa Serekali ina upungufu mkubwa wa Wataalam hao hasa katika Kisiwa cha Pemba ambpo alisema hivi sasa tayari Wizara hiyo imeomba kupatiwa ajira zaWataalam 40 ili angalau kupunguza tatizo hilo.


Alisema kuwa sababu kubwa inayochagia kuwepo kwa ukosefu wa Wataalamu hao hasa kwa upande wa Pemba, ni pale Bibi Shamba anapoolewa na Mume kutoka Unguja huomba uhamisho wa kumfuata mumewe.      

Post a Comment

0 Comments